‎Rafiki Yangu….

‎Alichopenda zaidi ilikuwa pipi. Kila aliponunuliwa pipi, alikuwa na furaha.
‎Lakini alipokua, pipi zikageuka kuwa simu, viatu vya bei, na maisha ya kuigiza kwenye mitandao.

‎Kitu kimoja hakikubadilika alikuwa bado hajui thamani ya pesa.
‎Mama yake alimsomesha shule nzuri.
‎Lakini hakumfundisha elimu ya fedha.

‎Makala hii itakuonyesha kwa nini ni muhimu kuanza kufundisha watoto elimu ya fedha wakiwa bado wadogo na jinsi unavyoweza kuanza leo, hata kama wewe si mtaalamu wa pesa.

‎Mwanao anaweza kuwa mtoto wa tofauti.
‎Anajua kuweka akiba.
‎Anaelewa thamani ya kazi.
‎Anaweza kupanga matumizi yake mwenyewe.
‎Anaweza kuanzisha biashara ya kuwauzia watoto wenzake vitu vya shule.

‎Ana mwelekeo wa kuwa huru kifedha kabla ya miaka 25.
‎Na yote yanaanzia na mafunzo madogo unayompa leo.

‎Wazazi wengi wanaanza kufundisha watoto wao masuala ya fedha wakiwa na miaka 6 tu.
‎Na matokeo ni ya kushangaza.
‎Mtoto wa miaka 10 ana bajeti yake.
‎Mtoto wa miaka 13 ana akaunti ya akiba.

‎Mtoto wa miaka 15 tayari anauza bidhaa mtandaoni.
‎Si kwa sababu ni “kwa bahati.” Ni kwa sababu walifundishwa.

‎Elimu ya fedha kwa mtoto wako haimaanishi kumpeleka darasani.
‎Inaanza kwa hatua ndogo kama hizi:

‎Mfundishe kutofautisha “nataka” na “nahitaji.”

‎Mpe fedha kidogo, mfundishe kuigawa kwenye matumizi, akiba, na msaada.

‎Mpe changamoto ya kuweka akiba kwa lengo maalum (kama kununua toy au kitabu).

‎Mshirikishe kwenye maamuzi madogo ya kifamilia kuhusu fedha.

‎Mpatie hadithi za watoto kuhusu pesa (vitabu, video, au michezo).
‎Unachofanya hapa ni kumjengea msingi wa maisha ya kiuchumi yenye busara.

‎Usisubiri mtoto akue ili uanze kumfundisha fedha.
‎Anajifunza kwa kukuangalia sasa.

‎Na kila siku inayopita bila elimu hii ni siku ya hasara kwa maisha yake ya baadaye.
‎Chukua hatua leo:
‎Anza kwa mazungumzo madogo, mifano midogo, na maamuzi madogo.
‎Kwa sababu kesho ya mtoto wako inajengwa leo.

‎Usimwachie dunia imfundishe mwanao kuhusu fedha maana dunia hufundisha kwa uchungu.

‎Fursa ni yako.
‎Wakati ni sasa.
‎Mfundishe pesa, kabla pesa haijamfundisha yeye.

‎Anway, kama bado hujathibitisha ushiriki wa uzinduzi wa program ya Nguvu Ya Buku Toto.

Imebaki Siku Ya Leo Tu!

Yaani ndio siku ya mwisho.

‎Kwahiyo wahi nafasi yako Sasa,

Kwa Ku‎tuma Ujumbe NATAKA NGUVU YA BUKU TOTO

‎Kwenda 0756694090.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Mkufunzi Ramadhan