‎Rafiki yangu,
‎Watu wengi wanapenda mafanikio…
‎Lakini wachache wako tayari kulipa thamani yake.

‎Wanataka maisha mazuri, pesa nyingi, heshima, uhuru…
‎Lakini wanataka yote hayo bila kutoa kitu cha thamani.

‎Huu ndio ukweli mchungu:
‎Kila mafanikio makubwa yana thamani fulani uliyoitoa.

‎Si uchawi, si bahati.
‎Ni gharama.
‎Na si lazima iwe pesa inaweza kuwa muda, nidhamu, maumivu, kujifunza, au hata kukataliwa.

‎ Watu Wanapenda Matokeo, Sio Safari

‎Tazama watu wengi mitaani.
‎Wanakataa kulala masaa machache, kusoma, lakini wanataka UTAJIRI.
‎Wanataka kufungua biashara, lakini wakipata changamoto ya kwanza wanakata tamaa wanaacha.

‎Wanataka kuwa bora, lakini hawako tayari kupitia maumivu ya ukuaji.

‎Wanataka matunda bila kupanda mbegu.
‎Na hapo ndipo ndoto nyingi hufia njiani.

‎Mafanikio Hayaji Kwa Bahati

‎Ukiwaona waliopiga hatua kubwa, usidhani walibahatika.
‎Wamelipa bei kimya kimya.
‎Walilala wakiwa wanapanga, walipoamka walichukua hatua.

‎Wengine walikataliwa, wakachekwa, wakasahauliwa,
‎Lakini hawakukata tamaa.

‎Walijua kitu kimoja muhimu sana:
‎Kuna thamani lazima utoe kabla ya mafanikio kuonekana.

‎Tatizo ni kwamba, wengi wanadanganywa na mitandao.
‎Wanamuona mtu amefanikiwa, wanadhani ni short cut.

‎Hawajui nyuma yake kuna machozi, kukatishwa tamaa, majaribu, na bidii isiyo na mwisho.

‎Ndiyo maana leo unaona watu wanachoka mapema.
‎Wanakata tamaa haraka, kwa sababu hawakujua mafanikio ni vita, si zawadi.

‎Unalipa Kabla Ya Kupokea

‎Rafiki yangu, hakuna kitu cha bure duniani.
‎Kila mafanikio unayoyaona, kuna mtu amelipa gharama yake.

‎Mwanafunzi anayeongoza darasani, amelipa kwa kusoma usiku.
‎Mjasiriamali anayeuza sana, amelipa kwa kujaribu mara nyingi bila kukata tamaa.

‎Mtu mwenye utulivu wa akili amelipa kwa kuacha mambo yasiyo na maana.

‎Swali ni Je! Wewe upo tayari kulipa nini kwa mafanikio unayotaka?

‎Suluhisho Sio Bahati Ni Thamani Unayotoa

‎Unataka mafanikio ya kweli?
‎Anza kutoa thamani kwanza.
‎Toa zaidi ya unachotarajia kupokea.

‎Saidia watu.
‎Jifunze.
‎Kua mwaminifu.
‎Fanya kazi kwa bidii hata kama hakuna anayekuona.

‎Mafanikio ni matokeo ya kile unachotoa, sio cha kile unachotamani.

‎Namkumbuka kijana mmoja niliyezungumza naye mwaka jana.
‎Aliniambia, Kaka Ramadhani, nimechoka. Nimefanya biashara miezi sita bila mafanikio.

‎Nikamuuliza swali moja tu:
Ni thamani gani umetoa kwa wateja wako hadi sasa?

‎Akanyamaza.
‎Alikuwa anauza, lakini hakuwa anasaidia.

‎Anapost, lakini hajengi uhusiano.
‎Anaomba watu wanunue, lakini hawajui kwa nini wanapaswa kufanya hivyo.

‎Tulianza kufanyia kazi sehemu moja tu kujenga thamani kabla ya kuuza.
‎Baada ya miezi mitatu, alianza kupokea wateja wapya kila wiki.

‎Leo ananiambia, Kaka, sasa najua mafanikio ni matokeo ya thamani niliyojenga, si bidhaa nilizonazo.

‎Hakuna mafanikio bila gharama.
‎Kila unachotamani, kina bei yake.
‎Na kadri unavyotoa thamani zaidi, ndivyo mafanikio yako yanavyokukaribia haraka.

‎Usiogope kutoa.
‎Usiogope kusubiri.
‎Usiogope kulipa gharama.

‎Kwa sababu gharama ni mlango wa mafanikio yako ya kudumu.

‎Ukitaka kuelewa kwa kina kanuni za kweli za mafanikio,
‎na kujua namna ya kujenga maisha yenye thamani, mafanikio, na utulivu wa ndani,

‎Soma kitabu hiki kipya kinachotikisa watu wengi,

FALSAFA YA MAISHA YA MAFANIKIO

‎Ndani yake utajifunza:

‎Siri ya watu wanaofanikiwa kimya kimya

‎Kwa nini wengine hukwama hata wakiwa na juhudi

‎Namna ya kulipa thamani sahihi bila kuumia

‎Na jinsi ya kuishi maisha yenye kusudi, heshima, na utajiri wa kweli.

‎Usiache siku ipite bila kusoma kitabu hiki.
‎Kwa sababu wakati wengine wanasubiri bahati,
‎watu wachache wanajifunza jinsi ya kujenga mafanikio kwa kutoa thamani.

‎Pata nakala yako ya FALSAFA YA MAISHA YA MAFANIKIO sasa:

‎Kwa kubonyeza hapa 👇
‎👉 https://wa.link/eqqp80

‎Karibu.
‎ 0756 694 090

‎PS: Jenga thamani, mafanikio yatakufuata.