‎Rafiki Yangu,

‎Kuna wakati maisha yanakupiga ngumi usiyoitarajia.
‎Unapoteza kazi.

‎Unasalitiwa.
‎Unakataliwa.
‎Unajitahidi lakini matokeo huyaoni.

‎Na hapo ndipo wengi hukata tamaa.
‎Wengine hukaa na kulia usiku kucha.
‎Wanajiona wameshindwa.

‎Wanahisi dunia imewaacha nyuma.

‎Lakini hebu nikuulize swali moja, rafiki…

‎Je, kulia kunabadilisha kitu?
‎Je, machozi yamewahi kulipa kodi?
‎Je, huzuni imewahi kuandika ukurasa mpya wa maisha yako?

‎Watu wengi hawajui kwamba maumivu si adui ni mwalimu.
‎Tatizo ni kwamba wengi wanashindwa kutafsiri somo lake.

‎Wanalia badala ya kusikiliza.
‎Wanajilaumu badala ya kujifunza.
‎Wanajificha badala ya kujijenga.

‎Hapo ndipo tofauti inapoanzia kati ya waliolia na waliotumia akili.

‎Waliolia walipoteza nguvu.
‎Lakini waliotumia akili walitawala maumivu yao, wakayageuza kuwa mafuta ya kusukuma maisha mapya.

‎Unajua kinachouma zaidi?
‎Ni pale unaona mtu ambaye mmepitia maumivu yanayofanana,

‎…lakini yeye ameyatumia kupanda juu,
‎na wewe bado upo hapo hapo,

‎…na unajiuliza Kwa nini mimi?

‎Ni kama dunia inakuonyesha picha ya vile ungepaswa kuwa,
‎…kama tu ungeamua kuamka badala ya kulia.

‎Kama tu ungeamua kutumia akili badala ya hasira.
‎Kama tu ungeamua kuona fursa badala ya huzuni.

‎Maumivu si hukumu. Ni changamoto.
‎Swali ni utayatawala, au yatakutawala?

‎Usidanganyike na maneno ya mitaani..

‎Eti subiri tu, bahati yako itafika.

‎Hapana!
‎Hakuna bahati inayofika bila akili kufanya kazi.
‎Hakuna maumivu yanayopotea kama hujayatawala.

‎Na hakuna mafanikio bila nidhamu ya kiakili.

‎Watu wanaofanikiwa sio wale wasio na maumivu,
‎…bali ni wale wanaotumia akili kuyageuza kuwa nguvu.

‎Hivyo acha kusubiri huruma.
‎Haitaokoa maisha yako.
‎Kitu pekee kitakachokutoa hapo ulipo ni mtazamo mpya wa kiakili.

‎Ukijua namna ya kutawala maumivu yako unakuwa na nguvu ya ajabu.
‎Unaanza kuona mbali.

‎Unaanza kujenga mipango mipya.
‎Unaanza kuvutia mafanikio, kwa sababu akili yako imezoea kusimamia hisia zako.

‎Kila tatizo linakuwa kama gym.
‎Kila changamoto inakuimarisha misuli ya ndani.

‎Ndipo unagundua:
‎Maumivu sio mwisho ni mwanzo wa toleo jipya la wewe bora zaidi.

‎Nakumbuka kijana mmoja aliwahi kuniambia,

Kaka Ramadhan, nilipoteza kila kitu. Biashara, mpenzi, na hata marafiki.

‎Nilimtazama na kumuuliza, Na baada ya hapo ulifanya nini?” ‎ ‎Akanijibu kwa tabasamu: ‎Nilikaa chini, nikaandika maumivu yangu kama ramani.
‎Nilijifunza kosa lilikuwa wapi.

‎Nikaweka akili yangu kufanya kazi siyo kulalamika.
‎Leo, maumivu yale ndiyo yamenifanya niwe mtu ninayeongoza timu yangu,
‎na ninasaidia wengine kujijenga tena.*

‎Nilijua pale maumivu yakitawaliwa, yanazaa nguvu mpya.

‎Rafiki yangu,
‎acha kutumia machozi kama silaha.
‎Yatumie kama maji ya kupunguza moto wa hasira ndani yako.

‎Wakati wengine wanalia,
‎wewe kaa kimya tafakari.
‎Chukua somo, jifunze, geuza huzuni yako kuwa ngazi ya kupanda juu.

‎Usikubali maumivu yakutawale.
‎Yatawale kwa akili.

‎Tumia falsafa ya ustoa kujitawala kwanza, kabla ya kuutawala ulimwengu.

‎Soma kitabu hiki kipya cha
‎FALSAFA YA USTOA, Ili ujitawale Mwenyewe, kisha Uitawale Dunia.

‎Kitabu hiki ndio ramani ya kujenga akili imara, moyo thabiti, na maisha yasiyotetereka.

‎Usikimbie maumivu yajue, yashinde, uyatumie.

‎👉 Sasa ni zamu yako kutawala maumivu yako kabla hayajakutawala wewe.

‎Unakipata hapa 👇 kwa ofa

https://wa.link/524kl0

‎Karibu.
‎0756694090.