Kwenye maisha, lazima kuna watu utawakera, hata kama lengo lako ni kumfurahisha kila mtu, bado hutaweza kufanya hivyo.
Hivyo chochote unachofanya kwenye maisha, jua kuna watu utawakera, kuna watu watakupinga na kukataa kwa kile unachosimamia.
Lengo lako halipaswi kuwa kutokuwakera watu au kukubaliwa na kila mtu, hilo haliwezekani. Lengo lako linapaswa kuwa kuyaishi maisha yako, huku ukijua kuna watu utawakera kwa kuishi hivyo.
Ukichagua kuweka juhudi kwenye kazi zako utawakera wavivu wasiopenda kuweka juhudi na ukichagua kutokuweka juhudi utawakera wale wanajituma.
Unapokazana kumridhisha kila mtu, unaishia kutokumridhisha yeyote, unapokazana usiwakere wengi, unaishia kuwakera wengi zaidi.
Amua leo ni watu gani uko tayari kuwakera katika kuyaishi maisha yako, ili wanapokereka na kukulalamikia, unawapuuza kabisa badala ya kuumizwa na malalamiko yao.
Mimi nimeamua kuwakera wote wasiopenda kujifunza na kujaribu vitu vipya, wale wanaoona usomaji wa vitabu hauna maana, nawakera kweli kweli, kwa sababu naamini kutoka ndani ya nafsi yangu kwamba kama mtu hajifunzi, hasa kwa kusoma vitabu, basi anachagua kuwa mjinga na kujizuia kupiga hatua.
Nimeamua kuwakera wale wote wanaoamini na kutafuta njia za mkato za mafanikio, wanaoamini kuna namna ya kupata mafanikio makubwa bila kuweka kazi na muda. Kutoka ndani ya moyo wangu naamini hicho kitu hakipo, na yeyote anayekiamini najua bila ya shaka kwamba anajipotezea muda wake.
Nimeamua kuwakera wale wote wanaoamini kwenye ushirikina na imani nyingine zisizokuwa na uthibitisho, naamini kwenye sayansi na sheria za asili, ambazo zimeufanya ulimwengu kuweza kwenda mpaka sasa. Chochote kinachoenda kinyume na sheria hizo za asili, huishia kuumia. Anayeamini kwenye ushirikina na imani nyingine za aina hiyo, kama uchawi, majini, ramli na mengine, namuona ni mtu ambaye bado anaishi kwenye zama za kale.
Kuna wengi nawakera, lakini hayo makundi matatu niliyoyashirikisha hapo juu, ndiyo yenye wengi na ambayo napambana nayo kila siku.
Je wewe umechagua kuwakera watu gani? Shirikisha kwenye maoni hapo chini.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Dr. Makirita Amani,
Asante kocha kwa ukurasa huu wa leo.
Nimeamua kuwakera watu kwa makindi kama yafiatayo
Wanaoamini kikifunza ni mpaka ikatunukiwe cheti baada ya kukaa darasani rasmi,ili hali karne tunayoishi tuna urahisi wa kijifunza chochote kupitia mtandaoni,na kwa mtu ninaamin maarifa yoyote nitakayokua nayataka nitaweza kujifunza na kuelewa.
Nitawakera wale wote wanaopenda kuwa waoga kwenye kazi na nyanja zingine katika maisha kwa kutokikibali kuwa wa kawaida kama vile jamii imekiweka katika mabano ya watu kufanana.
Nitawakera wote ambao hawaoni umuhimu wa kiwaza na kufanya uwekezaji wa muda mrefu,kwa kutokikimbilia njia za kutaka kifanikiwa haraka kwa kitumia njia nyepesi ili kupata haraka.
Nitawakera wanaoamini kufanikiwa inahitaji elimu kubwa ya darasani,na kuitegemea hiyo kwa maisha nakitegemea kuishi maeneo maarifu hapa nchini ambayo yalianza kuendelea mapema.
LikeLike
Hongera Hendry kwa kuchagua watu hao wa kuwakera katika kuishi misingi sahihi kwako.
LikeLike
Nimeamua kuwakera wale wote wanaofanya kazi kimazoea, kutosimamia sheria na haki ipasavyo na kupindisha ukweli wa mambo ili wajinufaishe wenyewe.
Nitawakera wale wote wanaojipendekeza kwa viongozi ili waweze kupewa nafasi za upendeleo wasizo stahili.
Nitawakera wote wanaoamini kuwa lazima utoe rushwa ndipo uweze kufanikisha mambo yako.
Asante sana Kocha kwa makala hii.
LikeLike
Safi sana Datius.
LikeLike
safi sana Datius kwa misingi uliyoamua kujiwekea.
LikeLike
Kwa kweli kocha mimi nimeamua kuwakera wote wasio amini katika mabadiliko makubwa, mtu akiamua kutoka ndani ya moyo wake anaweza kuwa anavyotaka kuwa.
Mimi naamini akili ni zao la juhudi na mafanikio pia ni zao la juhudi, kuna wanao kujitambua mapema katika kutimiza wajibu wao na kuna wanaochelewa kujitambua katika kutimiza wajibu wao.
Eti wale wanaojitambua mapema wanaonekana wana uwezo wa kutenda makubwa kuliko waliochelewa kujitambua.
Juhudi pekee ndio itamwamua mtu awe wa aina gani, mimi nilimaliza darasa la saba nikiwa simo hata kwenye orodha ya wanafunzi bora 50, hivyo jamii iliamini kuwa sina akili maana hata nikiwa kidato cha kwanza nilipa alama 4 kati ya 100 katika somo la kingereza ila baada ya kujitambua kuwa siweki juhudi na sitimizi wajibu wangu nilianza kujisomea kwa juhudi na nikahitimu kama mwanafunzi ninayeongoza somo la kingereza kwa kuongea na kufaulu darasani.
Sasa wengi wanaamini et ukiwa umevuka miaka 18 ni ngumu sana kujifunza lugha mpya, nikiwa na miaka 19 nilianza kujifunza lugha ya kichina ambayo ndio lugha ngumu kuliko zote duniani na niliweka juhudi kubwa mno ambapo baada ya mwaka mmoja nilitunukiwa tuzo ya utendaji bora katika mafunzo ya lugha ya kichina kwa tanzania bara na visiwani na kupewa udhamini wa masomo yani 4yrs full funded scholarship kwenda kusoma nchini china.
Kwa sasa naongea kichina kwa kasi ya ajabu na nimekuwa tu mchina wa mwanza.
Pia naamini utajiri ni sayansi ambapo kuna kanuni zikizingatiwa mtu lazima awe tajiri na hakuna kitakacho mzuia, hivyo nimeamua kuwakera wote wasio amini katika hilo.
Yani nitaongea kichina mpaka iwe kero kubwa kwa wasio amini katika juhudi kubwa za kila siku, na nitaendelea kuiishi misingi ya utajiri ili niendelee kabisa kuwakera wanaomini katika miujiza bila kufanya kazi na kuiishi misingi ya utajiri na imani za kishirikina,hawa nitaendelea kuwakera mno.
Nawakera mno wanao amini kuwa ili ufanikiwe kifedha lazima kuwe na mtu wa karibu au mwanafamilia aliyefanikiwa wa kukupa sapoti ili na wewe utoke..ninajitoa mimi mwenyewe kwa maarifa sahihi na association sahihi na wala sio kwa sapoti ya ndugu au kumtegemea mwanafamilia wa karibu.nawaacha wakazane na yao na mimi nakazana na yangu
Mimi naamini naweza kuwa vile ninavyotaka kuwa, nikita kuwa mhandisi nakuwa, nikitaka kuwa daktari nakuwa au vyovyote ninavyota kuwa.nimeamua kuwa tajiri na nitakuwa
Nikitaka kuwa mjapani wa mwanza nakuwa, nikitaka kuwa P square wa mwanza nakuwa na hata nikitaka kuwa nani wa afrika nakuwa.
Kwa kweli wapo wengi ninao wakera
Asante kocha
LikeLike
Hongera sana Alex, maisha yako ni somo kubwa kwa wengine, endelea kupambana kuishi kwenye misingi hiyo na utafika mbali sana.
LikeLike
Alex hongera sana,ni vitu ambavyo umevifanya si vya kawaida kabisa na hatua ulizochukua si za kawaida,hongera sana kuna somo pana kutoka kwako kweli.
LikeLike
Asante Sana kocha, nami nimeamua kuwakera wale wote wanaoishi na kufikiri kuwa hawawezi kuishi bila kutegemea ajira. Ninawakera wale wote wanaosema huwezi kufanikiwa kwenye maisha bila kupita njia za mkato. Ninawakera wale wote wanaojiona ni wanyonge na ambao hawaki kujifunza ili kugundua uwezo wa mkubwa ulio ndani yao.
LikeLike
Vizuri Tumaini.
LikeLike