2967; Haifai kwangu.
Rafiki yangu mpendwa,
Tofauti kubwa ya watu waliofanikiwa na walioshindwa ni hii; waliofanikiwa wanaona suluhisho kwenye kila tatizo, wakati walioshindwa waliona tatizo kwenye kila suluhisho.
Waonyeshe waliofakiwa njia fulani yenye matokeo mazuri kwa wengine na wataona jinsi gani njia hiyo inaweza kuwafaa na wao pia.
Lakini mwonyeshe aliyeshindwa njia fulani yenye matokeo mazuri kwa wengine na watakuonyesha kwamba haiwezi kufanya.
Watakuambia wazi; “Hiyo njia inaweza kufanya kazi kwa wengine na ikawanufaisha, lakini kwa upande wangu haiwezi kufanya kazi kwa sababu…. “
Hapo watakuorodheshea sababu nyingi za kwa nini njia hiyo haiwezi kufanya kazi kwao.
Na watakuwa wanajivunia kabisa hilo wanalofanya, wakiona ni jambo la kishujaa.
Hiyo haina tofauti na mtu mwenye kiu, ambaye anaelezwa kuna maji ambayo wengine wanakunywa, kisha yeye anasema hayo maji yanaweza kuwafaa wengine ila siyo yeye.
Cha haraka utakachopata kwenye hayo majibu ni huyu kiu haijamkamata kweli kweli.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwa wale wanaochagua kanuni za mafanikio, wanakuwa hawana kweli kiu ya mafanikio.
Kila unapoona mtu anasema kinachofanya kazi kwa wengine kwake hakitaweza kufanya kazi, jua hapo umekutana na mtu asiye na kiu ya mafanikio.
Anakuwa na uvivu, uzembe au ujinga, lakini hataki kukiri hayo.
Kwa mwenye kiu hasa ya mafanikio, atafanyia kazi kila njia hata kama hana uhakika nayo, kwa sababu anajua ni bora apotee kuliko kubaki pale alipo ambapo siyo anapopataka.
Anajua njia yoyote itakuwa na msaada kuliko kutokutumia njia kabisa.
Kinachofanya wengi wasingizie njia fulani haziwezi kufanya kazi kwao ni kutokutaka mabadiliko.
Mafanikio yanataka mtu awe tayari kuleta mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yake.
Mabadiliko yoyote yale huwa yanaumiza, wakati matokeo yake siyo ya uhakika.
Wenye mioyo myepesi huwa hawawezi kuyakabili mabadiliko hayo, hivyo huona njia pekee ni kuyakataa.
Kila unapojiambia njia fulani inaweza kufanya kazi kwa wengine ila kwako haiwezi kufanya kazi, jiulize ni uvivu, uzembe au ujinga unaokusumbua?
Kwa sababu kama huna njia unayotumia, njia yoyote ni nzuri kwako kuanzia.
Ni kweli hupaswi kufuata kila njia kama msaafu, utakwenda ukiiboresha kulingana na hali yako.
Lakini njia ni njia, inafanya kazi kwa kila mtu kama inafanyiwa kazi kwa uhakika.
Kwa kila unachojifunza kwa wengine, acha mara moja tabia ya kujiambia hakifai kwako. Badala yake jiulize kinafaaje kwako?
Kwa sababu njia ya kuelekea kwenye mafanikio ni kama ilivyo njia ya kwenda kwenye kisima cha maji, iko wazi kwa kila mtu, ila siyo wote watakaoitumia.
Ni rahisi kuona kila kitu ni kigumu na hakiwezekani kwetu.
Ni rahisi kuchukulia hali zetu ni za kipekee sana ambazo haziwezi kukabiliwa na njia zilizopo.
Lakini hayo yote ni kujitesa na kujichosha, ni kuyafanya mambo yawe magumu kuliko yalivyo kwa uhalisia wake.
Kama kweli unataka kufanikiwa, usitafute tatizo kwenye kila suluhisho au kila njia.
Badala yake ona njia kwenye kila tatizo.
Na kama huoni njia kabisa, angalia ni njia gani ambayo wengine wanatumia na kuwa tayari kuitumia kwa kuboresha zaidi kulingana na hali yako.
Misingi ya mafanikio ni ile ile kwa kila mtu na kila sekta. Kuna hatua za tofauti zinazopaswa kuchukuliwa kulingana na hali husika, lakini misingi ni ile ile, haibadiliki.
Kuikataa misingi hiyo ni kuonyesha jinsi gani huna kiu kubwa ya mafanikio.
Na ni bora ukiri hilo ili ijulikane moja, kuliko kujificha kwenye kichaka cha haiwezi kufanya kazi kwangu.
Sema njia fulani haiwezi kufanya kazi kwako kama tayari unayo njia nyingine inayokupa matokeo bora kabisa.
Lakini kama huna njia ya kukutoa pale ulipo sasa, ambapo hunaridhika napo, kamata njia yoyote inayokuja mbele yako na ifanye ikufanyie kazi.
Kila kitu kinafanya kazi kama kitafanyiwa kazi.
Acha maneno na visingizio na ufanye.
Mambo yote mazuri yako upande wa pili wa kufanya na siyo kwenye maneno au visingizio.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Upo sahihi sana kocha imenitia nguvu pia nimejifunza zaidi
LikeLike
Weka kwenye matendo.
LikeLike
Kama kweli ninataka kufanikiwa ninapaswa kutotafuta tatizo kwa kila suluhisho au njia.
LikeLike
Tafuta suluhisho la kila tatizo na siyo tatizo la kila suluhisho.
LikeLike
Njia ni moja kwa watu wote kilichobakia ni maamuzi ya kufuata njia hiyo
LikeLike
Kabisa,
Kutaka njia nyingine ni kujichelewesha.
LikeLike
Ahsante sana kocha, nitaona suluhisho katika kila tatizo
LikeLike
Safi sana.
Mtazamo sahihi huo wa kukuwezesha kuvuka chochote.
LikeLike
Kuona suluhisho kwenye kila tatizo ni jambo sahihi kwenye kufikia mafanikio kwenye maisha kwa ujumla wake mpana.
LikeLike
Kila kitu kinafanya kazi kama nitafanyia kazi. Asante Kocha.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Hakika.
Tusitafute tatizo kwenye suluhisho, bali tutafute suluhisho kwenye tatizo.
LikeLike
Mafanikio yanataka mtu awe tayari kuleta mabadiliko makubwa sana kwenye maisha yake. Asante sana Kocha Dr.Makirita Amani
LikeLike
Mabadiliko makubwa mno, ambayo hayajazoeleka kabisa.
LikeLike
Asante Kocha,
Siwezi/haiwezekani mara nyingi ni mbinu tu ya kuficha uvivu, uzembe na ujinga wetu.
LikeLike
Hatutaki tu kujiambia ukweli, na hilo linatupoteza zaidi.
Ni bora kuukabili ukweli, inakuwa mahali pazuri pa kuanzia.
LikeLike
Asante kocha,jambo kubwa ni kufanya kazi na kuacha visingizio.
LikeLike
Visingizio haviishi,
Visingizio haviingizi fedha.
Tuzalishe matokeo,
Tuachane na visingizio.
LikeLike
Mabadiliko yanaumiza sana na hayana uhakika na ndiyo maana wengi wanayakwepa. Asante Kocha
LikeLike
Sisi tuwe tayari kwa maumivu ili tuyakabili mabadiliko na tuweze kufanikiwa.
LikeLike
Nitaangalia suluhisho kwa kila changamoto iliyoko mbele yang
LikeLike
Vizuri, uzuri kila tatizo tayari lina suluhisho, ni wewe kulijua na kulifanyia kazi ili kuweza kupata matokeo ya tofauti.
LikeLike
Katika kila njia kuna changamoto ni bora kufuata njia yoyote kuliko kutokuwa na njia ahsante sana kocha
LikeLike
Vizuri, angalia suluhisho na siyo changamoto.
LikeLike
Naacha maneno,sababu na visingizio, nafanyia kazi kila njia Ili inifanyie kazi.
LikeLike
Vizuri,
Visingizio ni vitamu kuvitoa, lakini havinaga matokeo yoyote.
Tuachane navyo mara moja.
LikeLike
Ni bora nifuate njia yoyote ile kuliko kuendelea kusimama palepale na kusubiri
LikeLike
Hakika,
Hata ukipotea, angalau utakuwa umejua ni njia ipi haifanyi kazi ili usiirudie tena.
LikeLike
Kama sina njia ninayoifanyia kazi,nitaanza na njia yyote !
LikeLike
Kuwa kwenye mwendo, hata kama uelekeo siyo sahihi ni bora kuliko kutokuwa kwenye mwendo kabisa.
LikeLike
Kwa kila unachojifunza kwa wengine, acha mara moja tabia ya kujiambia hakifai kwako. Badala yake jiulize kinafaaje kwako?
LikeLike
Hakika,
Kama kinafanya kazi kwa wengine, kuna namna kinaweza kufanya kazi na kwako pia.
LikeLike
Kukataa kila njia ni kukataa mafanikio
LikeLike
Ukikataa angalau uwe na mbadala.
Sasa kama huna mbadala kabisa, unakuwa umejichelewesha wewe mwenyewe.
LikeLike
Kama huna njia ya kuanzia njia yoyote ni nzuri kwako kuanzia
Asante sama
LikeLike
Kabisa, ni bora upotee kuliko kuendelea kukaa mahali pamoja bila mwendo.
LikeLike
Njia ya kuelekea kwenye mafanikio ni kama ilivyo njia ya kwenda kwenye kisima cha maji, iko wazi kwa kila mtu, ila siyo wote watakaoitumia.
Ahsante Kocha.
LikeLike
Kuijua njia na kuitumia ni vitu viwili tofauti.
LikeLike
Kila unapojiambia njia fulani inaweza kufanya kazi kwa wengine ila kwako haiwezi kufanya kazi, jiulize ni uvivu, uzembe au ujinga unaokusumbua
LikeLike
Hakika,
Tunayaficha sana hayo na kusingizia njia haifanyi kazi.
LikeLike
Huo ni ugonjwa mkubwa sana kwetu hasa kwa ndugu na wafanyakazi wetu ukiwaambia fuata hii njia watakuambia haiwezekani kwangu wakati hata kujaribu tu hajajribu na hana njia nyingine anayotumia tumelemewa sana na uvivu na uzembe mimi nina mdogo wangu kabisa nimemuimbia hadi nimeamua kumuacha abaki na uzembe wake maana yeye kila kitu hawezi
LikeLike
Ni mtazamo mbaya na wa kukwamisha ambao wengi wanaukumbatia.
LikeLike