3056; Unajivuruga mwenyewe.
Rafiki yangu mpendwa,
Kutokana na ugumu na changamoto za safari ya mafanikio, watu wengi huwa wanatafuta watu wa kuwapelekea lawama pale mambo yao yanavyokwenda tofauti na matarajio.
Hapo watu huona wazi kwamba wamevurugwa na wengine ambao wamefanya tofauti na walivyotarajia.
Lakini huo siyo ukweli, hakuna mtu yeyote yule anayekuvuruga kwenye mambo yako.
Ukweli ni kwamba inajivuruga wewe mwenyewe.
Na unajivuruga kwa matarajio makubwa unayokuwa nayo, ambayo hayaendani na uhalisia.
Ni vigumu sana kumvuruga mtu ambaye anaupokea uhalisia kama ulivyo na kuutumia kuboresha safari yake ya mafanikio.
Watu wa aina hiyo hawalazimishi dunia iende kama wanavyotaka wao, bali wanaenda na dunia vile inavyokwenda na kubadilika kulingana na matokeo yanayopatikana.
Watu imara kwenye safari ya mafanikio ni wale wanaoichukulia safari yao kama wajibu wao wa msingi.
Wanajua kama watafanikiwa au kushindwa hayo yote ni juu yao wenyewe.
Watu wanajivuruga sana wao wenyewe na kujizuia kufanikiwa kwa kutaka dunia iende kama wanavyotaka wao.
Pale mambo yanapokwenda tofauti na matarajio, watu hao huona kama wamesalitiwa.
Wanachokuwa wamesahau ni jinsi ambavyo mambo mengi wanayofanya yapo nje ya udhibiti wao.
Chukua mfano mtu amekutukana au kukuibia. Kwa haraka haraka unaweza kuona mtu huyo amekuonea.
Lakini huo siyo ukweli. Ukweli ni kwamba mtu huyo anakuwa amekuonyesha uhalisia wake.
Sasa wewe kumlaumu mtu kwa kukuonyesha uhalisia wake ni sawa na kumlaumu mbwa kwa kubweka. Mbwa huwa wanabweka, ndiyo asili yao.
Kadhalika, wezi huwa wanaiba na wasiojali huwa wanatukana.
Badala ya kumlaumu mtu kwa kuona amekuvuruga, unapaswa kufurahia, kwa sababu amekuonyesha uhalisia wake.
Tangu hapo, utakuwa unaenda naye kwa tahadhari.
Nirudie kwa msisitizo, ni vigumu sana kumvuruga au kumkwamisha mtu ambaye anapokea uhalisia kama ulivyo badala ya kutaka uhalisia uwe vile wanavyotaka wao.
Kwa maneno mengine, ukitaka utulivu (na furaha) kuwa na mategemeo madogo sana kwa wengine au vitu vingine vilivyo njie ya uwezo wao.
Hawakazani kutaka mambo yawe rahisi kama wanavyotaka wao, badala yake wanakazana kuwa imara ili waweze kukabiliana na ugumu wowote wanaoweza kukutana nao.
Nguvu ya kweli kwenye maisha ni zao la kupokea uhalisia kama ulivyo. Ni kuwa imara na kutokuyumbishwa na chochote kile kinachotokea, hata kiwe kizuri au kibaya kiasi gani.
Kukubali uhalisia ndiyo hatua ya kwanza na muhimu kwenye safari ya mafanikio.
Somo kubwa sana tunaloondoka nalo hapa ni kuchagua kuyaishi maisha yako, kujitoa kwa kila namna kwenye kufanya kazi na kuyapokea matokeo kama yanavyokuja kwako kisha kuboresha zaidi.
Kama hulazimishi mambo yaende kama unavyotaka wewe, hakuna kitakachoweza kukuangusha au kukuvuruga.
Kukubali na kupokea uhalisia kama ulivyo haimaanishi kukata tamaa na kuona hakuna unachoweza kufanya.
Badala yake inamaanisha uwezo wako ni wa juu sana kiasi cha kuweza kutumia kila aina ya matokeo unayoyapata kuboresha zaidi safari yako ya mafanikio.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Uwezo wa kupokeaa uhalisia kama ulivyo ni ujasiri mkubwa sana.Ni nguvu kubwa kabisa mtu anayoweza kuwa nayo.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Nguvu ya kweli kwenye maisha ni zao la kupokea uhalisia kama ulivyo. Ni kuwa imara na kutokuyumbishwa na chochote kile kinachotokea, hata kiwe kizuri au kibaya kiasi gani.
Kukubali uhalisia ndiyo hatua ya kwanza na muhimu kwenye safari ya mafanikio.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Ninapokea kila aina ya matokeo yanayokuja kwenye maisha yangu na kuyatumia kujiboresha zaidi katika kupambania ndoto zangu kubwa nilizonazo kwenye maisha,na sitavurugwa na yeyote au chochote kile .
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
NITAJIBORESHA ZAIDI NA KUPAMBANIA MAONO NA KUSUDI LANGU HAPA
DUNIANI BILA KUVURUGWA NA CHOCHOTE KINACHOTOKEA KWANGU.
asante kocha.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Hakuna mtu yeyote yule anayenivuruga bali mimi peke yangu najivuruga.
LikeLike
Kujua hivyo kunasaidia sana.
LikeLike
Kukubali na kupokea uhalisia kama ulivyo haimaanishi kukata tamaa na kuona hakuna unachoweza kufanya.
Badala yake inamaanisha uwezo wako ni wa juu sana kiasi cha kuweza kutumia kila aina ya matokeo unayoyapata kuboresha zaidi safari yako ya mafanikio.
Asante sama
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Asante sana, nitaupokea uhalisia kama ulivyo.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nitahakikisha sijivurugi kwa kuwa nimegundua hamna Mtu wowote anaeweza kunivuruga Zaid ya Mimi mwenyewe
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Nitaacha kuwalaumu watu kwakuonesha uhalisia wao bali nitakuwa makini dhidi yao
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
“Nirudie kwa msisitizo, ni vigumu sana kumvuruga au kumkwamisha mtu ambaye anapokea uhalisia kama ulivyo badala ya kutaka uhalisia uwe vile wanavyotaka wao.
Kwa maneno mengine, ukitaka utulivu (na furaha) kuwa na mategemeo madogo sana kwa wengine au vitu vingine vilivyo njie ya uwezo wao”
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani.
LikeLike
Karibu sana.
LikeLike
Asante kocha,nitajitahidi kuweka nguvu kubwa kwenye kazi na sio kutoa lawama kwa watu wengine,ili nifanikiwe inanipaswa kuweka bidii zaidi.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Ni vigumu sana kumvuruga au kumkwamisha mtu ambaye anapokea uhalisia kama ulivyo.
ASANTE KOCHA
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Kukubaliana na kupokea uhalisia kama ulivyo maana yake una uwezo wa juu sana wa kutumia kila matokeo unayopata kuboresha safari yako ya mafanikio.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Kukubali uhalisia ndiyo hatua ya kwanza na muhimu kwenye safari ya mafanikio.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Nitaukubali na kuupokea uhalisia kama ulivyo na sitavurugwa na kitu chochote.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
kama unataka furaha(utulivu),kuwa na mategemeo machache toka kwa wengine,haijalishi ni mtu wa muhimu kwako kiasi gani tegemea machache.
usikasirike kutukanwa bali mtu kaonyesha uhalisia wake alivyo.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Kuupokea uhalisia kama ulivyo itakuwa muhimu kwangu, Asante sana kocha kwa Falsafa hii.
LikeLike
Karibu sana.
LikeLike
Asante sana kocha kwa makala mazuri kwa kweli hii imenibadilisha kifikra na kimtazamo kwa hiyo nitaupokea uhalisia kama ulivyo pia nitapunguza mategemeo mingi
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Tukubaliane na uhalisia na tuwe imara ili tusijevurugwa na yatakayotokea na yakitokea yawe ni fundisho kwetu
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Nakubaliana na kupokea uhalisia kama ulivyo ili kuwa na utulivu
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
nguvu ya kweli kwenye maisha ni kuupokea ukweli kama ulivyo
LikeLike
Hakika.
LikeLike