‎Rafiki Yangu Mpendwa,

‎Unajua nini kinauma?
‎Mtoto wako anaenda shule kila siku…
‎Anakazana…
‎Lakini hawezi hata kuweka akiba ya buku.

‎Sio kwa sababu hana hela.
‎Ni kwa sababu hajawahi kufundishwa.
‎Na hata wewe hujawahi kumfundisha.

‎Wengi wetu tunadhani watoto ni wadogo sana kufundishwa fedha.
‎Wengi tunasema:
Watapata tabu bure.
Wangojee wakue kwanza.

‎Lakini hiyo ndio sumu kubwa zaidi.

‎Umemwona mtoto wa jirani yenu?
‎Ana miaka 12 tu… lakini ana “Akaunti” yake.
‎Anaandika kila hela anayopata.
‎Anajua kutumia na kuweka akiba.

‎Mtoto Wako Je?
‎Anachukua elfu moja…
‎Anaimaliza yote na bado anakwambia nitumie tena.

‎Na unamtumia.
‎Kila siku.
‎Mwaka mzima.
‎Miaka kadhaa…

‎Mpaka kesho hajui thamani ya buku.
‎Hajui kusema nitahifadhi.

‎Na bado unamuita smart?

‎Kibaya zaidi ni kwamba watu wazima wengi ndo kwanza wana matatizo ya fedha.
‎Na wanadhani watoto wao watajifunza wakikua.

‎Mbona na wewe umekua lakini bado hela hazikutoshi?

‎Unawapenda watoto wako?
‎Basi wape zawadi ambayo hawataisahau maisha yao yote:

‎Maarifa ya fedha.

‎Kuanza ni rahisi kuliko unavyodhani.
‎Anza kwa kumfundisha kutunza buku moja.
‎Moja tu.
‎Kwa wiki.
‎Kwa mwezi.
‎Hata kwa siku.

‎Tengeneza kopo au boksi.
‎Kiite Boksi La Buku.
‎Mwambie:
Kila siku utaweka buku hapa ndani, mwisho wa mwezi tutajua umekomaa kiasi gani.

‎Mfanye ajivunie akiba yake.
‎Mfanye ahisi kama mjasiriamali.
‎Mpe changamoto za “ku-save.”
‎Utaona tabia yake inabadilika.

‎Fedha ni mchezo wa akili.
‎Na akili inaanza mazoezi mapema.

‎Nilikutana na mama mmoja Keko, Dar.
‎Mtoto wake wa miaka 10 alikuwa anauza keki za shilingi 500.

‎Anachukua faida yake, anaweka buku kila jioni kwenye kopo.
‎Mama alimfundisha baada ya kushindwa kulipa ada mwaka mmoja.

‎Baada ya miezi 6…
‎Yule mtoto alikuwa na Tshs 120,000.
‎Alijinunulia viatu.
‎Alichangia ada.
‎Akaambiwa: Wewe utakuwa mtu mkubwa sana.

‎Na ni kweli.
‎Leo yule mtoto ana ndoto za kuwa “mfanyabiashara maarufu duniani.”
‎Na anaiamini.
‎Kwa sababu anaona inavyowezekana.

‎Usisubiri watoto wakue.
‎Waanze sasa.
‎Buku moja kwa siku ni shule kubwa kuliko darasa.

‎Tengeneza “Mpango wa Kuokoa Buku” nyumbani kwako leo.
‎Kila mtoto aanze.
‎Hii siyo hadithi, ni maisha.

‎👉 Anza leo, kabla mtoto wako hajaanza kukulaumu kesho.

‎Anyway, kama bado hujaweka oda ya kitabu hiki kipya cha NGUVU YA BUKU TOTO,

‎Basi nafasi yako hii hapa 👇 kabla ya tarehe 9.

‎Ni hapa 👉https://wa.link/2x7eqq

‎Karibu.
‎Imetoka Kwa Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,
‎Mkufunzi Ramadhan Amir