‎Hapo Zamani,

Samson alikuwa kijana wa kawaida aliyeamua kuanzisha biashara ya kuuza vitenge Kariakoo, Dar es Salaam.

‎Hakuwa na mtaji mkubwa, lakini alikuwa na ndoto kubwa ndoto ya kuinua familia yake,

‎Kutoka kwenye maisha ya kukopa hadi maisha ya kutajwa kwenye semina kubwa kama ‘mfanyabiashara aliyefanikiwa.’

‎Lakini kuna kitu kilimkosesha usingizi ni kwamba biashara yake ilikuwa haikui.

‎Kila siku alifungua duka, aliketi akisubiri wateja, lakini pesa haikufuata jasho lake.

‎Siku moja akiwa kwenye daladala, alisikia vijana wawili wakizungumza kwa furaha kuhusu jinsi walivyoongeza mauzo kwenye biashara zao kwa msaada wa kitabu kimoja kinachoitwa CHUO CHA MAUZO.

‎Mmoja alisema:

‎“Bila hiki kitabu, nisingejua kuwa neno dogo tu kama ‘Habari Njema’ linaweza kuvutia mteja kuliko punguzo.”

‎Samson alishtuka. Kitabu? Mauzo? Hayo siyo mambo aliyowahi kuyapa uzito.

‎Alikuwa akiamini kwamba mauzo yanakuja tu kama bahati au kwa kupumguza bei.

‎“Nani ana muda wa kusoma vitabu?”

‎ Alijiambia. “Mbona mimi nataka pesa sasa hivi, siyo masomo.”

‎Lakini wiki hiyo hiyo alipoteza mteja mkubwa aliyekuwa tayari kununua mzigo wa laki mbili.

‎Mteja alimwambia:

‎“Samahani kaka, sikuhisi kama unajua unachouza.”

‎Maneno hayo yalimchoma kama msumari wa moto.

‎Samson alimkumbuka kijana mmoja anayeitwa Musa, aliyekuwa na duka jirani.

‎Musa alikuwa na foleni ya wateja kila asubuhi.

‎Akamwendea na kumuuliza:

‎“Kaka, unatumia uchawi gani?”

‎Musa alicheka na kumpa nakala ya kitabu cha CHUO CHA MAUZO.

‎“Soma hiki. Hiki ndicho kilichonigeuza kutoka kuwa muuzaji hadi kuwa mshauri wa wateja.”

‎Samson alianza kusoma. Kurasa ya kwanza akisema:

‎“Wateja hawataki tu bidhaa, wanatafuta suluhisho.

‎Ukiweza kuzungumza na hisia zao, utauza zaidi ya bidhaa utauza matumaini.”

‎Alijifunza mbinu za kuuliza maswali sahihi, kutumia lugha ya kuhamasisha, kuandaa ofa za kuvutia, na kutengeneza uhusiano wa kudumu na wateja.

‎Hakuona mabadiliko ya haraka.

‎Ilibidi apambane na woga wa kuzungumza, kukumbana na wateja wagumu, na kuacha tabia ya kusema “Karibu kaka” bila maana.

‎Lakini siku moja, mteja mpya alikuja na Samson alitumia mojawapo ya mbinu kutoka kitabu kile.

‎Badala ya kuuliza “Unataka kitenge gani?”
‎Aliuliza:

‎“Unatafuta kitenge kwa ajili ya kukivaa kwenye hafla ya aina gani?”

‎Mteja alitabasamu.

‎“Kwa harusi ya mdogo wangu. Wewe ni tofauti.”

‎Akanunua vitambaa vitatu bila kuomba punguzo.

‎Miezi mitatu baadaye, Samson alikuwa tayari kuongeza duka la pili. Lakini janga lilitokea:

‎Ghafla washindani walitoa bei za chini sana sokoni.

‎Wateja wengi walienda kwao. Samson akakaribia kukata tamaa.

‎Lakini alifungua tena kurasa za mwisho za CHUO CHA MAUZO na kukumbushwa:

‎“Unaposhindwa kuuza kwa bei, uza kwa thamani.”

‎Akaanza kuongeza huduma ya kufungasha zawadi, kutoa ushauri wa mitindo kwa wateja, na kutuma ujumbe wa shukrani kwa kila mteja aliyenunua.

‎Sasa Samson hakuwa tu muuzaji wa vitenge alikuwa mshauri wa mavazi ya hafla.

‎Biashara yake ilikua kwa kasi ya ajabu.

‎Mapato yake yakaongezeka MARA MBILI ndani ya miezi sita.

‎Samson alianza kushiriki mafunzo kwa wafanyabiashara wengine wadogo.

‎Akawaambia:

‎“Siri haipo kwenye bidhaa, ipo kwenye akili yako na akili inachochewa na maarifa.

‎Na maarifa haya niliyapata kwenye kitabu cha CHUO CHA MAUZO.”

‎Leo hii, Samson ni mfanyabiashara mkubwa, ana wafanyakazi, duka la mtandaoni, na anaandaliwa kuhudhuria semina ya kimataifa.

‎Yote yalianza pale alipoamua kuchukua kitabu na kukisoma.

‎Kama wewe ni mfanyabiashara na unajiuliza “Nifanye nini ili niuze zaidi?”

‎Jibu linaweza kuwa si bidhaa mpya, si duka kubwa zaidi bali ni maarifa mapya.

‎👉 Chukua kitabu cha CHUO CHA MAUZO leo.

‎👉 Geuza biashara yako kuwa shujaa wa sokoni.

‎Anyway, kama bado hujapata kitabu hiki, unaweza kuweka oda yako hapa 👇

https://wa.link/6pruxn

‎Karibu.
‎0756694090.

‎Rafiki Yako Anayekupenda Na Kukujali Sana,

‎Ramadhani Amir