Hii Ndio Siri Ya Watu Wenye Utulivu Wa Ajabu!

‎Watu Wachache Wanaijua, Lakini Inawafanya Waishi Maisha Yasiyotikisika

‎Rafiki Yangu,

‎Kuna watu wanapitia changamoto kubwa…
‎Lakini bado wanatabasamu.
‎Hawakimbii.
‎Hawapigi kelele.
‎Wanakaa kimya, wanatulia, wanatafakari.

‎Unashangaa, Anawezaje kuwa mtulivu wakati mambo yameharibika hivi?

‎Wakati wengine wanapoteza mwelekeo,
‎wengine wanabaki imara kama mwamba.

‎Siri yao ni moja tu..
‎ Wamejifunza kutawala akili zao.
‎Si kwa sababu maisha yao ni rahisi
‎bali wameamua kuwa watulivu hata wakati dunia inawapigia kelele.

‎Utulivu hauji kwa bahati.
‎Ni maamuzi ya ndani.
‎Ni nidhamu ya akili.
‎Ni ujuzi wa kujitawala.

‎Lakini wengi wanashindwa hilo.
‎Wanakasirika haraka.
‎Wanachoka mapema.
‎Wanavunjika moyo kwa jambo dogo.
‎Wanakuwa watumwa wa hisia zao.

‎Kuna watu wanaamka na furaha asubuhi,
‎lakini saa tatu tu wanakuwa wameshajaa hasira.
‎Kila kitu kinawakasirisha.
‎Kila mtu anawaudhi.

‎Na mwisho wa siku,
‎wanajiona wamechoka, wamepotea, wamevunjika ndani.

‎Maisha yao ni kama redio yenye kelele.
‎Hawatulii.
‎Hawana amani.

‎Hiyo ndiyo sababu watu wengi hawafiki walikopanga.
‎Sio kwa sababu hawana maarifa,
‎bali kwa sababu hawajui utulivu wa ndani unavyofanya akili ifanye kazi vizuri.

‎Usidanganywe na mawazo ya mitaani.
‎Eti mtu mtulivu ni dhaifu.
‎Eti kukaa kimya ni kuogopa.
‎Hapana!

‎Utulivu ni nguvu.
‎Kimya ni silaha.
‎Mtu mwenye utulivu anaona mbali kuliko wenye kelele.

‎Watu wengi wanadhani nguvu ni kupiga kelele,
‎kuonesha hasira, au kushindana na kila mtu.
‎Lakini ukweli ni kwamba…
‎nguvu ya kweli ni kujua lini usiseme kitu.
‎Ni kujua namna ya kufikiri kabla ya kutenda.

‎Mtu mwenye utulivu hajali nani anamchokoza.
‎Anajua thamani ya amani yake ya ndani.

‎Sasa hebu jiulize,
‎unawezaje kuwa na utulivu huo wa ajabu?

‎Kwanza, anza kujijua.
‎Tambua kinachokukasirisha, kinachokuvunja moyo, kinachokukengeusha.
‎Ukishakijua, unakimilikisha.

‎Pili, jifunze kukaa kimya.
‎Wakati unahisi unataka kujibu haraka kaa kimya.
‎Wakati unahisi unataka kulipiza kisasi tulia.
‎Hapo ndipo nguvu inaanza kukua.

‎Tatu, fanya maamuzi ukiwa umetulia.
‎Hasira, huzuni, au hofu hazina uwezo wa kuona mbali.
‎Lakini akili iliyotulia inaona fursa hata katikati ya giza.

‎Utulivu ni kama macho ya ndani.
‎Unapoona wazi, unaishi vizuri.

‎Namkumbuka rafiki yangu mmoja, Said,
‎alikuwa anapoteza mteja mkubwa kila alipokasirika.
‎Kila mara akihisi kudharauliwa, anajibu kwa ukali.
‎Na mwisho wa siku, anajikuta ameharibu dili.

‎Siku moja aliniambia,
Bro Rama, nimechoka kuharibu kila kitu kwa hasira zangu.

‎Tukakaa, nikamfundisha kitu kimoja…
Tulia kwanza. Hasira zikipita, ndipo utajua cha kusema.

‎Akanisikiliza.
‎Miezi michache baadaye, akanipigia simu.
‎“Bro, kile ulichoniambia kimeniokoa.

‎Nilipotulia, niliweza kusaini mkataba ambao nilikuwa nakaribia kuharibu.
‎Sasa najua, utulivu ni nguvu kuliko maneno.

‎Leo, Said ni mmoja wa watu wanaoheshimika kazini kwake.
‎Watu wanamwambia, Bro, una utulivu wa ajabu!

‎Anacheka tu, anajua siri yake ni moja alijifunza kujitawala.

‎Rafiki yangu,
‎usitafute utulivu kwa kutoroka matatizo.
‎Tafuta utulivu kwa kujijua.
‎Kwa kuutawala moyo wako.
‎Kwa kuamua kuwa imara hata wakati mambo ni magumu.

‎Hiyo ndio siri ya watu wenye utulivu wa ajabu.
‎Wamejifunza kwamba nguvu ya kweli haiko kwenye misuli,
‎bali iko kwenye akili tulivu.

‎Kwa sababu mtu mwenye utulivu wa ndani,
‎anaweza kushinda vita yoyote ya nje.

‎Anyway kujifunza zaidi,

‎Soma kitabu hiki kipya cha
FALSAFA YA USTOA

‎Kitabu hiki kinakufundisha siri ya kutawala akili yako,
‎kutuliza moyo wako,
‎na kuishi maisha yenye amani hata katikati ya kelele za dunia.

‎Kupata kitabu hiki bonyeza hapa 👇

https://wa.link/524kl0

‎Karibu.
‎0756694090.

‎PS: Utulivu Ni Nguvu. Jifunze Kuimiliki Leo.