Rafiki Yangu,

‎Kila mtu ana hisia.
‎Hasira, huzuni, woga, wivu, tamaa, furaha… vyote hivyo ni sehemu ya maisha.

‎Lakini tatizo ni moja wengi hawajui namna ya kuzitawala.
‎Wanazifuata kila zinapowasukuma.
‎Wakikasirika, wanatenda vibaya.
‎Wakihisi wivu, wanaharibu uhusiano.
‎Wakihisi tamaa, wanafanya maamuzi ya kipumbavu.

‎Hisia ni kama moto ikitawaliwa, inapika chakula;
‎isipotawaliwa, inachoma nyumba.

‎Na hapa ndipo wengi wanapotea.
‎Wanachukulia hisia kama mwongozo,
‎wakati ziliumbwa kuwa miongozo midogo tu ya ndani, si dira kuu ya maisha.

‎Ndio maana wengi wanajuta baadaye.
‎Wanakuja kusema, Nilikasirika nikasema vibaya,
‎au Nilihisi hivyo, nikafanya uamuzi mbaya.

‎Kuna watu leo wamepoteza kazi kwa sababu ya dakika tano za hasira.
‎Wengine wamepoteza ndoa kwa sababu ya siku moja ya wivu.
‎Wengine wameharibu ndoto zao kwa sababu walihisi wamechoka na wakaacha njiani.

‎Hisia zikitawala akili, akili hufa.
‎Na mtu anapopoteza uwezo wa kufikiri kwa utulivu,
‎anaweza kuharibu kila kitu alichokijenga kwa miaka mingi… ndani ya sekunde chache tu.

‎Fikiria mara ya mwisho ulipofanya maamuzi ukiwa na hasira.
‎Ulijisikiaje baada ya dakika 30?
‎Ndiyo, majuto.
‎Huo ndio mtego unaowakamata wengi.

‎Tunaishi katika dunia ambayo watu wanakuambia,
Fanya unachohisi.
Follow your heart.
Usijizuie, jisikie tu.

‎Lakini ukweli ni kwamba si kila unachohisi ni sahihi.
‎Hisia ni kama mawimbi ya bahari zinakuja, zinapanda, zinashuka.
‎Ukiziendesha bila dira, utakosa mwelekeo na utazama.

‎Huwezi kuishi kwa kufuata kila unachohisi,
‎kwa sababu hisia hubadilika kila dakika.
‎Unachohitaji si kufuata hisia zako,
‎bali kuzisikiliza, kisha kuzitawala.

‎Kujizuia haimaanishi unajinyima,
‎inamaanisha unajilinda.

‎Nguvu ya kweli ipo kwenye utulivu wa ndani.
‎Kwenye uwezo wa kufikiri hata wakati moyo unachemka.
‎Kwenye uwezo wa kusema hapana hata wakati mwili unasema ndiyo.

‎Watu wachache wana hiyo nguvu.
‎Lakini wale wachache, ndio wanaofanikiwa zaidi.

‎Unapoanza kutawala hisia zako,
‎unaacha kuwa mfungwa wa mazingira.
‎Unaanza kuwa mtawala wa matokeo.

‎Hasira ikija unaitambua, si kuifuata.
‎Wivu ikija unajiuliza inanifundisha nini?
‎Huzuni ikija unaitazama kama mwalimu, si adui.

‎Kila hisia ikipita, unakuwa bora zaidi, si dhaifu zaidi.

‎Namkumbuka dada mmoja niliyemfahamu, aitwaye Mariam.
‎Alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na roho juu.
‎Anachukia haraka, anasema chochote, anafanya maamuzi papo kwa papo.

‎Siku moja akakasirika kazini, akaamua kuacha kazi bila mpango.
‎Wakati ule, alihisi ameshinda.
‎Lakini baada ya wiki mbili, akalia machozi.
‎Hakukuwa na kazi nyingine, hakukuwa na kipato, hakukuwa na amani.

‎Baada ya miezi michache, alijifunza kitu kikubwa:
Nilijifunza kuwa si kila unachohisi unapaswa kukifanya. ‎Maumivu yaliponifunza nidhamu, nilianza kufanikiwa.

‎Leo Mariam ana biashara yake.
‎Anasema maneno haya kila mara:
Hisia ni kama farasi ukizikalia vizuri, zinakupeleka mbali; ‎ukiziachia, zinakuangusha vibaya.

‎Rafiki yangu,
‎usiruhusu hisia zikupoteze tena.
‎Tawala hasira yako.
‎Tawala woga wako.
‎Tawala tamaa zako.

‎Kwa sababu mtu anayetawala hisia zake,
‎anaweza kutawala dunia yake.

‎Wakati wengine wanapotea kwa kufuata hisia,
‎wewe anza kujijenga kwa kuzitawala.
‎Utashangaa maisha yanavyoanza kukusikiliza.

‎Kujifunza zaidi..

‎Soma kitabu kipya:
‎FALSAFA YA USTOA,

‎Kitabu hiki kinakufundisha jinsi ya kushinda vita vya ndani.
‎Kinafundisha namna ya kutumia akili mbele ya hisia.
‎Na namna ya kujenga utulivu hata katikati ya misukosuko.

‎Unakipata hapa 👇

https://wa.link/524kl0

‎PS: Usiishi Kwa Kufuata Hisia Zako Anza Leo Kuzizidhibiti.
‎Hapo Ndipo Nguvu Yako Ya Kweli Ilipo.

‎Karibu.
‎0756694090.