Watu Wachache Wanaielewa, Lakini Inawapa Maisha Yenye Amani na Mwelekeo

‎Rafiki Yangu,

‎Kuna watu wanapitia changamoto kila siku…
‎Lakini bado wako cool.
‎Wana utulivu.
‎Wanafanya maamuzi kwa akili, si kwa hofu.

‎Wakati wengine wanapotea kwa presha,
‎wao wanatulia, wanapumua, na kufikiri.

‎Unashangaa, Wanafanyaje?
‎Kwa sababu kila kukicha dunia inawapigia kelele,
‎mambo yanagoma, presha zinapanda,
‎lakini bado hawaonekani kuchanganyikiwa.

‎Siri yao ni moja wanafahamu sayansi ya akili tulivu.
‎Wamejifunza namna ya kuishi bila kuruhusu kila kitu kuvuruga ndani yao.

‎Lakini ukweli ni kwamba wengi wetu hatujui siri hiyo.
‎Tunachanganyikiwa haraka.
‎Tunapoteza mwelekeo kwa jambo dogo.
‎Simu ikilia vibaya, moyo unadunda.
‎Ujumbe mmoja tu unaharibu siku nzima.

‎Unajikuta unaamka na amani,
‎lakini jioni unakosa hata pumzi.

‎Kila kitu kinakuuma.
‎Kila mtu anakukasirisha.
‎Kila tukio linakupeleka mbali na utulivu wako.

‎Unalalamika, unaumia, unachoka.
‎Unahisi dunia inakukaba.

‎Lakini ukweli ni huu dunia haitakoma kuwa na misukosuko.
‎Ila wewe unaweza kujifunza kuishi bila kuchanganyikiwa hata katikati ya kelele hizo.

‎Usiweke imani kubwa sana kwenye wazo la nitakuwa na amani nikishafanikiwa.

‎Hapana.

‎Amani ya kweli haianzii nje.
‎Inaaanzia ndani.

‎Watu wengi wanadhani utulivu ni matokeo ya maisha mazuri,
‎lakini kiukweli maisha mazuri ni matokeo ya utulivu.

‎Kama akili yako haijatulia,
‎hata ukipata pesa, utaumia.
‎Hata ukipata mafanikio, hutayaona.
‎Hata ukipata mapenzi, utakosa furaha.

‎Hii ndio sababu wengine wana kila kitu,
‎lakini bado wanaishi kama wamechanganyikiwa.

‎Sayansi ya kuishi bila kuchanganyikiwa inajengwa hatua kwa hatua.

‎Kwanza:

‎Jifunze kujisikiliza ndani yako.
‎Usikimbilie kujibu tafuta utulivu.
‎Wakati mambo yanaenda mrama, kaa kimya kidogo.
‎Acha akili yako ipumue.

‎Pili:

‎Jifunze kutenganisha tatizo na hisia zako.
‎Siyo kila unachohisi ndicho ukweli.
‎Wakati mwingine akili yako inahitaji muda wa kufikiri kabla ya kuchukua hatua.

‎Tatu:

‎Kumbuka si kila kitu kinahitaji majibu yako mara moja.
‎Wakati mwingine, kimya chako ndicho jibu bora zaidi.

‎Ukijua haya,
‎unaacha kuchanganyikiwa kwa vitu vidogo.
‎Unaanza kuona mambo kwa uwazi.
‎Na unajifunza kwamba nguvu yako kubwa ipo kwenye utulivu wako wa ndani.


‎Namkumbuka jamaa mmoja anaitwa Kelvin.
‎Kila siku alikuwa na stress kazini.
‎Wafanyakazi wanamkwaza, boss anamlaumu, mteja analalamika.
‎Kila siku ni kelele kichwani.

‎Siku moja akaenda likizo ya wiki moja.
‎Akiwa huko, alikaa kimya.
‎Hakujibu simu.
‎Hakutuma meseji.
‎Akaanza kuandika hisia zake kila asubuhi.

‎Alipoendelea, akagundua kitu kimoja kikubwa:
Nilikuwa naumia si kwa sababu ya kazi, ‎bali kwa sababu ya namna nilivyokuwa naifikiria.

‎Aliporudi, hakubadilisha kazi.
‎Lakini alibadilika yeye.
‎Akaanza kupanga siku zake vizuri,
‎akajifunza kusema hapana pale inapobidi,
‎na akaanza kuishi kwa utulivu.

‎Leo Kelvin ni mtu tofauti.
‎Wale waliokuwa wakimcheka kwa upole wake,
‎sasa wanamuuliza, Bro, unawezaje kubaki mtulivu hivi?

‎Rafiki yangu,
‎Kuishi bila kuchanganyikiwa si uchawi.
‎Ni sayansi.
‎Ni maamuzi.
‎Ni nidhamu ya akili.

‎Dunia haitapunguza kelele,
‎lakini unaweza kujifunza kusikia kimya chako ndani yake.
‎Na hapo ndipo nguvu ya kweli inapoanzia.

‎Usiruhusu mambo ya nje yakuvuruge.
‎Tawala akili yako, utatawala maisha yako.

‎Soma kitabu kipya cha
FALSAFA YA USTOA

‎Ujitawale Mwenyewe Kisha Uitawale Dunia.

‎Kitabu hiki kinakufundisha sayansi ya utulivu.
‎Namna ya kutumia akili yako kuishi bila kuchanganyikiwa,
‎…bila presha, na bila kupoteza amani yako ya ndani.

‎Anza leo kujenga akili isiyotikisika maisha yako yatabadilika milele.

‎Kukipata kitabu hiki, unaweza kubonyeza hapa 👇

https://wa.link/524kl0

‎Karibu.
‎0756694090.