Unapofanya uwekezaji au jambo lolote unashauriwa kuwa na malengo ambayo utakuwa unayafuata katika utekelezaji wako. Na ukifanya uwekezaji hasa katika hisa ni vyema ukawa na malengo ya kukaa na Hisa zako kwa muda Fulani. Uwekezaji katika Hisa unamanufaa ikiwa utawekeza kwa muda mrefu na utapata manufaa makubwa.

clip_image001

Kwanini uwekeze kwa muda mrefu?

Ukiwekeza kwa muda mrefu uwekezaji wako utakua kwa kiwango kizuri, uwekezaji wa kuanzia mwaka 1 au 2 au zaidi ni rahisi kwa mwekezaji kuona ukuaji wa uwekezaji wake katika ongezeko la thamani. Mara nyingi ongezeko la bei ni rahisi kulitambua katika uwekezaji wako ikiwa utawekeza kwa muda mrefu. Vile vile katika kipindi hicho ni rahisi kwa mwekezaji kupata gawio la mwaka au miezi sita.

SOMA; Kinachokufanya Ukwame, Na Uwe Na Maisha Magumu.

Ukiwekeza kwa muda mrefu unaondoa hatari ya kupata hasara, kama utafanya uwekezaji wa muda mrefu katika Hisa ni rahisi kuondoa hatari ya kupata hasara kutokana na kupanda na kushuka kwa bei za hisa. Bei za hisa hupanda na kushuka, kwa hiyo ikiwa utawekeza kwa muda mfupi ni rahisi kupata hasara kama utauza kipindi ambacho bei zimeshuka ndani muda mfupi.

Ukiwekeza kwa muda mrefu una nafasi nzuri ya kupata gawio, kama utawekeza kwa miezi miwili ni vigumu kupata gawio kwa kuwa kampuni nyingi hutoa gawio kila baada miezi sita au mwaka. Kwa mwekezaji ambaye atawekeza kwa muda mrefu ana nafasi nzuri ya kupata gawio na kunufaika na uwekezaji wake.

Muda ambao mwekezaji anashauriwa kuwekeza na kukaa na uwekezaji wake

Unashauriwa kuwekeza kwa muda wa mwaka 1 au zaidi na uwekeze katika kampuni zaidi ya moja. Ukiwekeza kwa mwaka mmoja au zaidi na kwa kampuni tofauti unazuia hatari ya kupoteza pesa yako na uwekezaji kukua kwa kiwango kizuri.

Mwandishi: Emmanuel Mahundi

Mawasiliano: emmanuelmahundi@gmail.com au 0714 445510

Kwa kujifunza zaidi tembelea www.wekezamtanzania,blogspot.com

SOMA; Siri Hii Itakusaidia Kuondokana Na Msongo Wa Mawazo Wa Kukosa Muda Katika Ulimwengu Huu Wa Utandawazi – 3