Habari za leo rafiki yangu?
Unajua leo ni lini? Leo ni tarehe 01/10/2016 hii ni tarehe mpya kabisa ya mwezi mpya ambapo mwaka unaelekea ukingoni. Leo tumeianza ngwe ya mwisho kabisa ya mwaka huu 2016. Ni ile robo ya nne ya mwaka 2016 tumekwenda kuianza leo. Unapoona tumefika ngwe ya mwisho, ni dalili kwamba mwaka siyo wetu huu. Mwaka unakaribia kutuaga. Hivyo basi kwa chochote ambacho ulikuwa umepanga kutimiza mwaka huu, ni muhimu sasa ukabadili kila mbinu kama bado hujaanza hata kukifanya.
Kwa wale ambao tulishiriki pamoja semina ya kuweka malengo mwaka huu 2016, na kuweka malengo ambayo walinishirikisha, tafadhali niandikie email kunijulisha umefika wapi na kama una changamoto yoyote ambayo inakuwa tishio kwako kufanikisha malengo yako.

Pia kwa wale ambao walijiunga kwenye program ya SUPERCOACHING, tuwasiliane ili kuboresha mikakati ambayo tulijiwekea kama bado mambo hayajakaa sawa kama tulivyokuwa tumepanga yawe. Kitu kimoja ambacho nakiamini ni hiki, chochote tunachotaka kwenye maisha yetu, kipo ndani ya uwezo wetu, ila tunahitaji kufanya zaidi ya uwezo wetu ili kuweza kukipata.
Rafiki yangu sasa nikukaribishe kwenye makala yetu ya leo ambapo tutakwenda kujadili jinsi ya kupata milioni ya ziada kila mwezi hata kama huna mtaji wa kuanzia kwa sasa. Lakini kabla hatujaingia huko, naomba nikumbushe haya machache.

Jana ilikuwa siku ya mwisho ya kupata ofa ya kitabu cha JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG, watu wote ambao walituma fedha na ujumbe wenye email zao walitumiwa kitabu kile kwenye email zao. Kama ulituma fedha na hujapata kitabu kwenye email yako basi tuma ujumbe wenye meseji ya udhibitisho wa kutuma fedha pamoja na email yako kisha utatumiwa kitabu mara moja. Unaweza kutuma ujumbe huo kwenye namba 0717 396 253 au 0755 953 887. Kama hukutuma fedha jana ili kupata kitabu hiko, unaweza kutuma leo tsh elfu 10 kwenye moja ya namba hizo pamoja na email yako kisha ukatumiwa kitabu hiko. Ofa imeisha jana rafiki yangu, usitume tena elfu tano, tuma elfu kumi. Karibu sana.

Kuna jambo moja muhimu naomba niliongelee kabla sijaingia kwenye mada ya leo. Jana mmoja wa msomaji na rafiki yetu alinipigia simu. Alikuwa na malalamiko kwamba tangu amejiunga na mtandao huu hajapokea mafunzo badala yake ni taarifa za kutuma hela ya kitabu tu. Nilikubaliana naye kwamba kwa wiki hii nimekuwa nawakumbusha wale wote ambao hawajapata kitabu kufanya hivyo. Lakini wiki iliyopita, kila siku kwa siku saba niliendesha semina ya blog bure kabisa ambayo kila mtu alikuwa na nafasi ya kuweza kushiriki semina ile. Na tangu mwaka 2013 nimekuwa natuma email kwa ninyi marafiki zangu, siyo kweli kwamba natuma email za kuuza vitu peke yake.

Kwa hiyo nilimshauri kama anaona anachopata ni matangazo pekee, basi akifika chini kwenye email kuna sehemu imeandikwa UNSUBSCRIBE, ukibonyeza hapo basi hutapata tena email yoyote kutoka kwangu. Na hili pia nataka niliseme kwa marafiki zangu wengine wote, kitu ambacho nakithamini mno ni muda wako, kuliko hata fedha yako. Sipendi kupoteza muda wako, na ndiyo maana najitahidi kadiri ya uwezo wangu kukuandalia maarifa bora, na kuhakikisha unayapata. Kama kwa namna yoyote utaona unapata matangazo kuliko unavyopata maarifa, basi shuka chini kabisa kwenye email, utaona sehemu imeandikwa UNSUBSCRIBE, ukibonyeza hapo unakuwa umejiondoa kwenye mfumo huu wa email. Sipendi nikupotezee muda wako, napenda uwe hapa kama kuna thamani unaipata kwenye maisha yako, kama hakuna basi hakuna sababu ya wewe kupoteza muda.

Baada ya wiki hii ya kuhakikisha kila rafiki yangu mwenye nia amepata kitabu cha blog, kuanzia kesho tutarudi kwenye ratiba yetu ya kawaida kwenye mfumo wa email. Kila jumapili tunakuwa na makala ya FALSAFA MPYA YA MAISHA, jumanne, ONGEA NA COACH, na alhamisi, kwa mwezi wote huu wa kumi nitakuwa nakukumbusha kuhusu semina ya MILIONI YA ZAIDA, ambayo nitakupa maelezo zaidi hapo chini. Hivi ndivyo tutakavyokwenda kwa mwezi huu wa kumi. Karibu sana rafiki yangu.

Pole rafiki, nimeandika mengi lakini muhimu. Karibu kwenye ujumbe wetu wa leo ambapo nakwenda kukueleza na kukukumbusha kuhusu semina ya MILIONI YA ZIADA.
Tumekuandalia semina inayoitwa MILIONI YA ZIADA, hii ni semina ambayo itafanyika kwa njia ya kuhudhuria kwenye ukumbi, tofauti na semina zangu ulizozoea. Kwenye semina hii walimu wanne, ambao wengine taarifa zao nitakuletea, tutakufundisha na kukupa mbinu za kuweza kuyatumia mazingira uliyopo sasa, kutengeneza milioni ya ziada kila mwezi.

Hii ni semina ambayo mtu yeyote ambaye yupo makini na maisha yake hapaswi kuikosa. Kwa sababu kama ambavyo wote tumekuwa mashahidi, kadiri siku zinavyokwenda, mambo yanazidi kuwa magumu. Hii ina maana kwamba, mbinu tulizokuwa tunatumia awali kwa sasa haziwezi kuleta matunda mazuri tena. Sasa tunahitaji kuja na mbinu mpya kama kweli tunataka kupata matokeo bora. Kupitia semina hii utajifunza mbinu hizo mpya ambazo utaweza kuzitumia kuboresha maisha yako, kwa kujihakikishia kipato cha ziada.

Semina hii itafanyika jumapili ya tarehe 30/10/2016 pale BLUE PEARL HOTEL, UBUNGO PLAZA. Tafadhali sana rafiki yangu, iwekee alama hiyo tarehe na usipange tukio jingine lolote katika tarehe hiyo isipokuwa kuhudhuria semina hii ya kipekee sana kwako. Na kama upo mkoani, anza kuweka ratiba yako vizuri ili uweze kusafiri na siku hiyo ya jumapili ya tarehe 30/10/2016 uwe dar kwa ajili ya kushiriki semina hii.

Ada ya kushiriki semina hii ni tsh 35,000/= na hapa ndipo pazuri sana. Nasema ni pazuri kwa sababu watu wengi wamekuwa wanatumia ada kama kigezo cha kushindwa kushiriki semina. Hivyo ili wewe rafiki yangu usikose semina hii nzuri ya kipekee, ili usiniandikie kwamba natamani kushiriki semina hiyo ila fedha sina, nimekuandalia mpango mzuri kwako ili kuweza kupata fedha hiyo.
Mpango huu utakuchukua siku 30, kuanzia lei tarehe 01 mpaka siku ya semina tarehe 30/10/2016, unachohitaji ni kila siku kuweka akiba ya angalau tsh 1,500/= unaweza hata kuweka tsh 2,000/= lakini hakikisha haipungui 1,500/=. Kila siku fanya hivi, swali ni je unawezaje kufanya hivi?

Anza kwa kupunguza gharama zozote ambazo umekuwa unaingia ambazo siyo za msingi. Mfano badala ya kununua maji ya kunywa kila siku, unaweza kuwa na chupa yako nzuri ya kubebea maji. Badala ya kunywa bia au soda kila siku, weka fedha hiyo akiba. Badala ya kununua vocha kila siku ambazo huzitumii kwa uzalishaji tunza fedha hiyo. Jaribu kwa siku hizi 60, uone unavyoweza kuokoa 1,500/= kila siku, utaona jinsi ambavyo maisha yako yataanza kubadilika.

Fanya hivi kila siku, na hakika utapata ada ya kushiriki semina hii ya kipekee. Hata kama hutaweza kushiriki semina hii, au hutashiriki kwa namna yoyote ile, bado nakusihi sana ufanye zoezi hilo, litakusaidia kuanza kushika hatamu ya maisha yako.

Semina ni tarehe 30/10/2016 rafiki, itunze tarehe hiyo. Ada ya kushiriki semina hii ni tsh 35,000/= rafiki, anza kuiandaa leo tarehe 01. Nina imani kubwa tutakutana kwenye semina hii na kwa pamoja tuweke mikakati ambayo italeta mapinduzi makubwa kwetu kifedha.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kwa ushauri na Coaching bonyeza maandishi haya kupata utaratibu.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea MTAALAMU NETWORK