Hakuna yeyote anayeweza kukosea mara zote au kupatia mara zote. Kila mmoja wetu kuna mambo anakosea na mengine anapatia.

Tunapaswa kuwa wanyenyekevu ili kujua wakati tunapokosea na pia kuweza kujifunza kwa wengine.

Kama unadhani wewe unapatia tu na wengine wanakosea tu, hutaweza kujifunza na mara zote utafanya makosa zaidi.

Hata saa iliyosimama, huwa inakuwa na majira sahihi mara mbili kwa siku.

Una mengi ya kujifunza kupitia wewe mwenyewe na kupitia wengine pia.

Ukurasa wa kusoma ni kuhusu marehemu alisema, fungua; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/02/16/2240

#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma