#SheriaYaLeo (181/366); Iga Maadili Yao.

Kufikiri na kusema kile unachotaka kusema kwa watu wote ni kukitafutia matatizo yasiyo na manufaa.

Watu wenye hekima wanajua kwamba wanapaswa kuonyesha tabia zinazoendana na wale wanaowazunguka.
Wanajua siyo lazima waamini kwenye mambo hayo.

Manufaa wanayopata ni kwa kufanya kile ambacho wengine wanafanya kwa nje, wanakuwa huru kufikiri kile wanachotaka kwa ndani.

Hawalazimiki kutetea maadili na misimamo yao kwa wale wasioielewa.
Kwa sababu hawawapi watu wasioelewa nafasi ya kujua maadili na misimamo yao.

Maana kila wanapokuwa nao, wanaiga maadili na misimamo yao.
Kwa kila jamii unayokuwa au kundi unalokuwa ndani yake, fanya kama wao wanavyofanya.
Kuonyesha misimamo yako ya tofauti ndani ya makundi ya aina hiyo ni kukaribisha mashambulizi ambayo hayana faida yoyote kwako.

Wengi hawapo tayari kufanya hivi kwa sababu wataonekana ni wanafiki.
Wanataka muda wote wafikiri, kusema na kutenda kwa namna wanavyotaka wao.
Hakuna anayeweza kukuona ni mnafiki kama unaonekana kufanya kile ambacho wao wanafanya pia.
Watu wanakuona ni mnafiki pale wanapoona unafanya tofauti na wao.

Kupata uhuru wa kufikiri na kufanya mambo yako, iga kwa nje kile ambacho wengine wanafanya.
Hilo litakuondolea usumbufu wa kujieleza na kujitetea kuhusu maadili na misimamo yako ya tofauti.

Sheria ya leo; Kuwa huru kufikiri na kufanya vile unavyotaka wewe ni kitu ambacho hakiwezekani kwenye jamii. Jifunze kuficha mawazo yako ya tofauti na pale unapokuwa kwenye jamii, waambie watu kile wanachotaka kusikia huku ukifanya kama wao wanavyofanya. Lakini ndani yako na ukiwa na watu wenye uelewa kama wako ndiyo upo huru kifikiri na kufanya vile unavyotaka wewe.

#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji