‎Kakaa/Dadaa Yangu…

‎Kuna uongo mmoja hatari sana unaoenezwa Kwenye jamii zetu…

‎Watu wanaambiwa mafanikio ni siku moja kubwa.

‎Siku moja utajikuta na gari.

‎Siku moja utakuwa na pesa za kukutosha.

‎Siku moja utahama mtaa.

‎Siku moja…

‎Siku moja…

‎Siku hiyo haiji bwana.

‎Mafanikio si sherehe ya ghafla.

‎Ni safari ya kila siku bila makelele.

‎Wewe unasema unataka kufanikiwa, sawa…

‎Lakini unalala hadi saa nne asubuhi.

‎Simu ndiyo bibi yako.

‎Series zimekuwa chakula cha akili yako.

‎Maisha yako yanaenda kwa “autopilot”.
‎Upo tu.

‎Ukisubiri muujiza.

‎Bro, Sister, hakuna muujiza bila jasho.

‎Hii dunia haitoi zawadi kwa wavivu.

‎Ina wanyonya.

‎Na inawatupa bila huruma.

‎Sikiliza vizuri…

‎Mafanikio ni mazoea madogo unayorudia kila siku.

‎Ni kuamka mapema, hata kama hupendi.

‎Ni kusoma ukurasa mmoja, hata kama huna mood.

‎Ni kupanga siku yako kabla haijaanza.

‎Ni kukataa vishawishi vidogo  kwa ndoto kubwa.

‎Wale wanaosema “take it easy, usijibane sana”

‎Ndiyo wale wale watakucheka ukifeli.

‎Wakupe pole usiku, mchana wakutangaze.

‎Usikubali!

‎Hata kama ni kwa dakika 15.

‎Soma, tafakari, panga.

‎Jifunze kitu kipya.

‎Andika ndoto zako.

‎Jikumbushe sababu zako.

‎Chapa kazi hata kama haionekani leo.

‎Hiyo ndiyo siri.

‎Mafanikio hujificha ndani ya maumivu ya kila siku.

‎Na mwishowe hutokeza kwa kishindo.

‎Mimi ni shahidi.

‎Nilianza kuandika bila jina.

‎Nilikuwa naandika status zinasomwa na watu wawili.

‎Nilikaa hadi usiku nikiandika makala kama hii bila malipo.

‎Wakati wengine wanalala, mimi nilikuwa naota nikiwa macho.

‎Leo hii…
‎Watu wananitafuta.
‎Wananilipa.
‎Wananiamini.

‎Lakini yote yalianza na ile siku niliyoamua kuamka mapema.

‎Siku niliyoamua… kila siku ni nafasi ya kufika mbali.

‎Na sitaki nisikie mtu anasema, “wewe ni bahati.”

‎Hapana.

‎Ilichongwa kwa jasho la kila siku.

‎Mafanikio ni kila siku.

‎Sio mwendo wa kusprint.

‎Ni marathon ya moyo, bidii, na nidhamu.

‎Usijilinganishe.

‎Jilinganishe na wewe wa jana.

‎Na hakikisha kesho, unamshinda huyo wa leo.

‎Leo umeamka sasa swali ni moja tu:

‎Utafanya nini?

‎Anyway,

‎Kama bado hujajiunga na wenzake makini kwenye huduma za ukocha, bonyeza hapa 👇 na utapewa utaratibu wa kujiunga.

https://wa.link/i2r67s

‎Karibu.
‎0756694090.
‎Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.