‎Kakaa/Dadaa Yangu…

‎Wengi Wanashindwa.
‎Watu wengi wanatamani sana kuwa na biashara zao.

‎Wanachoka kuamka asubuhi kwenda kazini kwa mtu.
‎Wanakasirika kuona pesa zao zikilipia ndoto za wengine.

‎Lakini kila wakitaka kuanzisha biashara, akili inagoma.

‎Nakujiambia…

‎“Mwanangu biashara inahitaji mtaji mkubwa…”

‎“Aaah, siku hizi biashara ni ngumu bana…”
‎“Bora nikatae tu, nisijiumize moyo…”

‎Unasikia hizo sauti?

‎Zinaonekana kama ushauri, lakini ni mtego.
‎Mtego wa ubaki pale pale.
‎Ukiwa na ndoto kubwa, lakini ukiishi maisha madogo.

‎Inaumiza sana,

‎Kwa sababu kila siku inaisha bila kupiga hatua yoyote.
‎Unaamka. Una scroll Instagram.

‎Unamuona jamaa yako wa zamani anaendesha gari mpya.
‎Anaposti “Nashukuru Mungu kwa neema.”

‎Unamjua vizuri kwamba hana hata degree.
‎Hakusoma sana kama wewe.

‎Lakini ana biashara. Ana uhuru. Anaishi maisha ya ndoto zake.

‎Wewe bado upo hapo unajiambia, “Siku moja nitaanza.”

‎Siku moja haiji. Mwaka unaisha. Maisha yanasonga.

‎Unakuwa mtaalamu wa kupanga, sio wa kuchukua hatua.

‎Na hapa ndipo watu wengi wanakosea.
‎Wanasubiri hali iwe sawa.
‎Wanasubiri mtaji wa milioni.
‎Wanasubiri mtu awashike mkono.

‎Hebu Nikuambie Ukweli,
‎Na Tuivunje Ile Imani Potofu.

‎Biashara haianzi na pesa.
‎Biashara haianzi na duka kubwa.
‎Biashara haianzi na mkopo wa benki.

‎Biashara inaanza na wazo + ujasiri + hatua ndogo.

‎Kama huwezi kuuza kitu cha buku, huwezi kuuza kitu cha elfu 10.

‎Kama huwezi kupata mteja mmoja, huwezi kupata mia.

‎Watu wanalala wakisubiri kuamka na mtaji.
‎Lakini hawajui hata namna ya kuuza idea zao.

‎Unataka biashara yako ikue?

‎Acha kufikiria sana. Anza kufanya.

‎Acha kutafuta approval ya watu.
‎Anza kutafuta mteja wako wa kwanza.

‎Sasa Sikiliza Nikuambie….

‎Na Hizi Hapa Ndizo Mbinu Zenyewe.

‎(a) Anza na kitu unachokielewa au unachokipenda.

‎Usianze kwa kufuata pesa. Anza kwa kufuata suluhisho unaloweza kutoa.

‎(b) Fanya utafiti.
‎Tafuta watu wenye shida hiyo.
‎Angalia wanahangaika na nini.
‎Uwauzie suluhisho.

‎(c) Tengeneza kitu cha bei rahisi.
‎Toa sample. Toa ladha ya huduma yako.
‎Watu waone thamani kabla hawajatoa hela.

‎(d) Tengeneza jina.
‎Tumia WhatsApp, status, Facebook, IG.
‎Simama kama mtu anayeaminika.

‎(e) Kua pole pole.
‎Kama leo unapata mteja mmoja, kesho wawili.
‎Boresha. Rudia. Panua.
‎Hapo ndipo biashara inapanuka.

‎Bado namkumbuka….

‎Dada Yangu Mary Alinifunza Mengi.

‎Mary alikuwa anauza maandazi kwa shilingi 100.
‎Watu walimcheka. Walisema, “Hii si biashara.”

‎Lakini alikuwa na kitu kimoja consistency.

‎Alikuwa analeta kwa wakati.
‎Anacheka na wateja.

‎Anatoa bonus kwa mteja wa tatu.
‎Miezi mitatu baadaye, alipata mteja wa catering.

‎Akapika kwenye harusi.
‎Akapata hela ya kuongeza mtaji.

‎Sasa ana duka la vyakula.
‎Ana wafanyakazi wawili.

‎Wale waliomcheka, sasa wanamuuliza anatoa kazi lini.

‎Biashara yake ilianza na mafuta ya buku tano na unga wa kilo moja.
‎Lakini aliweka moyo.
‎Aliweka ubunifu.
‎Aliweka tabasamu.

‎Sasa Ni Zamu Yako
‎Acha kuogopa.
‎Acha kungoja hali iwe “shwari.”

‎Anza na ulicho nacho.
‎Fanya vizuri kuliko wote.
‎Fanya kwa moyo.
‎Fanya kila siku.

‎Kumbuka Hii:
‎Biashara si ya matajiri.
‎Biashara ni ya wale waliochoka kusubiri.

‎Na kitabu kilichomfungua Dadaa Mary ni kitabu Kinachoitwa ELIMU YA MSINGI YA BIASHARA.

‎Kama unacho hongera na rudia kuisoma sura ya kwanza.

‎Lakini kama bado hujakipata bonyeza hapa 👇

https://wa.link/gr5iim

‎Karibu.
‎0756694090.
‎Hii Makala Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.