‎Kakaa/Dadaa….

‎Unajua shida kubwa inayowakumba wengi?
‎Wanaamka kila siku…
‎Wanakimbizana kama mchwa waliomwagiwa maji…

‎Lakini hawajui wanakimbilia wapi.

‎Kila siku ni kujituma…
‎Lakini mwisho wa mwezi, mfuko ni kama shimo la panya.
‎Kila mwaka unakatika…
‎Lakini hakuna mabadiliko ya maana.

‎Wengi wako kwenye ‘autopilot’ ya maisha.
‎Wanajisukuma tu.
‎Wakiamini ipo siku mambo yatajileta.
‎Mambo hayajileti. Wewe ndo lazima uyasogeze.

‎Hii Inatisha Kidogo…

‎Unaamka ukiwa na nguvu.
‎Unaota mafanikio.
‎Lakini kila jioni, unarudi na uchovu tu.
‎No progress.
‎No peace of mind.

‎Unasema utabadilika kesho.
‎Kesho ikifika, unafanya yaleyale.
‎Ni kama umefungwa pingu zisizoonekana.

‎Hii ni hatari sana.
‎Inaua ndoto zako taratibu bila kelele.
‎Alafu unakuja kushangaa:
‎“Mbona maisha yananizunguka?”
‎Ni kwa sababu hakuna mwongozo.

‎Kuna Uongo Mmoja Mkubwa…

‎Eti “kuwa na bidii, utafanikiwa.”
‎Wongo huo.
‎Watu wengi wana bidii kuliko hata gari la kubeba mawe.
‎Lakini wako pale pale.

‎Tatizo si bidii.
‎Tatizo ni kutokuwa na DIRA.
‎Hakuna ramani.
‎Hakuna mwongozo.

‎Na kama hujui unakokwenda…
‎Hutajua hata ukifika.

‎Sasa Sikiliza Vizuri…

‎Maisha yako yanahitaji mfumo.
‎Mfumo wa kuweka malengo.
‎Kujijua wewe ni nani.
‎Unataka nini.
‎Na kwa nini unakitaka.

‎Halafu?
‎Anza kupanga hatua ndogo ndogo.
‎Kila siku.
‎Kidogo kidogo hadi kikamilike.

‎Na muhimu zaidi, tafuta maarifa ya kweli.
‎Si porojo.
‎Maarifa ya watu waliopitia moto.
‎Walioungua.
‎Wakaamka.
‎Wakasimama tena.

‎Ngoja Nikupe Kisa Cha Huyu Bwana Mdogo Hapa…

‎Kuna Bwana Mdogo mmoja mtaani kwetu Anaitwa Baba T.

‎Miaka mitano iliyopita alikuwa anauza vocha na peremende stendi.
‎Maskini alikua anavaa viatu vilivyochanika…
‎Watu walimcheka.

‎Lakini kuna siku moja aliniambia:
‎“Bro, nimeshaamua. Sitaki kufa maskini. Nataka mafanikio ya ukweli.”

‎Akanunua daftari.
‎Akaandika malengo yake.
‎Akasoma vitabu.
‎Akatafuta mentor.
‎Akaanza kuandika kila kitu anachotumia.

‎Leo hii?
‎Ana duka lake la simu.
‎Anauza online.
‎Anatoa ushauri kwa vijana wengine.
‎Na bado ni yule yule – Baba T ila mwenye mwongozo mpya wa maisha.

‎Na Wewe Unaweza Kubadilika Leo…

‎Ukiamua, unaweza.
‎Ukiwa na mwongozo sahihi, maisha yanabadilika.
‎Unapunguza makosa.
‎Unafupisha safari ya mateso.
‎Unapanda ngazi haraka.

‎Chukua hatua.
‎Andika malengo yako.
‎Soma kila siku.
‎Tafuta watu wanaojua kuliko wewe.

‎Achana na kelele za mtaani.
‎Focus.

‎Maisha ni yako.
‎Na hakuna atakayeyaishi kwa niaba yako.

‎Unataka mafanikio ya kweli?
‎Tafuta mwongozo.
‎Fuata mfumo.
‎Jitahidi bila kusahau mwelekeo.

‎Maisha si bahati.
‎Ni maamuzi na maandalizi.

‎Kupata Mwongozo Uliomsaidia Baba T,

‎Bonyeza Hapa 👇

https://wa.link/x0i8o5

‎Karibu.
‎0756694090.
‎Hii Makala Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan Amir.