Habari rafiki?
Fedha ni moja ya maeneo muhimu sana ya maisha yetu, ukiondoa hewa ambayo tunaipata bure bila ya kulipia chochote, kitu cha pili kwa umuhimu zaidi ni fedha, kwa sababu bila fedha, huwezi kupata chochote kwenye maisha. Najua unajua hata kupata maji safi na salama ya kunywa, unahitaji kuwa na fedha. Hivyo hilo halina ubishi.
Pamoja na umuhimu huu mkubwa wa fedha kwenye maisha yetu, bado watu wengi wanateseka sana kwenye swala la fedha. Wapo watu ambao wanafanya kazi sana lakini bado fedha ni changamoto kubwa kwao. Wapo ambao wanatengeneza kipato kikubwa lakini baada ya muda maisha yao yanakuwa magumu sana. Na wapo wale ambao wamekazana kwenye kazi zao, wakaweka juhudi za kutosha, lakini siku moja wakaambiwa kazi hakuna tena na maisha yao yakawa magumu mno.
Yote haya yanasababishwa na kosa moja kubwa sana ambalo watu wengi wanafanya, kuwa na mfereji mmoja wa kipato. Mtu anakuwa na njia moja pekee ya kumtengenezea kipato. Anaizoea njia hiyo na kuitegemea, pale unapotokea changamoto na kipato kwenye njia hiyo kikakauka, ndipo matatizo makubwa yanapoanza.
Katika somo letu la video leo, nakwenda kukushirikisha umuhimu wa kuwa na mifereji mingi ya kipato. Popote pale ulipo kwenye maisha yako, ni muhimu sana uwe na mifereji mingi ya kipato, uwe na njia nyingi za kukuingizia kipato. Hii ndiyo njia pekee unayoweza kujitengenezea uhuru wa maisha yako.
Kujifunza kwa kina kuhusu hili, angalia somo hili zuri la leo. Unaweza kuangalia somo hili kwa kubonyeza maandishi haya, au ukaangalia moja kwa moja hapo chini.
Karibu sana ujifunze na uweze kuchukua hatua ili uweze kujijengea uhuru wa kifedha.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Kupata blog yako ya kitaalamu, unayoweza kuitumia kutengeneza kipato, BONYEZA maandishi haya.
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.