Habari za leo rafiki yangu?
Karibu kwenye kipindi chetu cha leo cha ONGEA NA COACH ambapo nimekuwa nakushirikisha video zenye mafunzo mbalimbali ya kukuwezesha kuwa bora zaidi na kuweza kufanikiwa. Nimekuwa nakusisitiza mara zote kwamba MAFANIKIO NI HAKI YAKO YA KUZALIWA, hakuna yeyote anayeweza kuichukua haki hiyo kwako.
Kwenye kipindi cha leo nimekushirikisha jambo muhimu sana kuhusu biashara.
Watu wengi ambao wamekuwa wanapanga kuingia kwenye biashara, wamekuwa wanauliza swali ambalo siyo sahihi. Swali lao ni je biashara ipi yenye mafanikio makubwa naweza kufanya?
Swali hili lina ndugu zake kama; wapi nikiweka fedha zangu baada ya miezi sita nakuwa nimetengeneza mara mbili?
Maswali yote hayo siyo sahihi na yamewapotosha wengi. Yamewafanya wengi kukimbizana na vitu ambavyo siyo sahihi kwao, kupoteza fedha na hata muda pia. Huku wakiacha biashara nzuri ambazo wangeweza kufanya na kufanikiwa sana.
Kwenye kipindi hichi nimekuonesha kwa kina aina ya biashara ambayo unaweza kuifanya na ukafanikiwa sana.
Kwenye kipindi hichi nimekueleza mambo mawili muhimu sana kuhusu biashara ambayo wengi hawajawahi kuambiwa na hawapendi kusikia. Kwa kujua hayo mawili tu, kunakutosha kufanya biashara yako kwa utofauti mkubwa.
Pia nimekupa hatua tatu muhimu za kuanza biashara yoyote ile unayoanza ambazo zitakuwezesha kuanza biashara sahihi na kufanikiwa pia.
Kupitia kipindi hichi cha leo, nimekuonesha wapi pa kuanzia na uanzeje, hata kama upo chini kabisa. nimekupa hatua kwa hatua uanzie wapi na ukueje zaidi.
Mwisho kabisa sijaacha kuzungumzia kuhusu mikopo kwenye biashara. Kwa sababu hii imewasumbua wengi na kuwaangusha. Hapa nimekupa tahadhari kubwa sana kuhusu mikopo na namna gani unapaswa kuwa makini nayo.
Kama upo kwenye biashara, au unapanga kuingia kwenye biashara, basi hichi ni kipindi kimoja ambacho unapaswa kukiangalia, na tena kukiangalia kwa umakini mkubwa. Kwa sababu yapo mambo mengi madogo madogo ambayo hutayasoma kwenye vitabu wala kuyapata kwenye ushauri wa biashara unaopewa na wengine.
Angalia kipindi hichi cha leo kwa kubonyeza maandishi haya, au kwa kuangalia moja kwa moja hapo chini iwapo kifaa chako kina uwezo huo.
Neno langu kwako ni moja tu, kila biashara ni nzuri kama tayari upo kwenye biashara. Acha kupoteza muda kujiuliza biashara ipi nzuri, ingia kwenye biashara na utaona namna ya kutengeneza biashara nzuri kwako.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu
Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea www.mtaalamu.net/patablog