‎Kakaa/Dadaa…

‎Unasema unataka kubadilisha maisha yako.

‎Unasema unataka pesa.

‎Unasema unataka mafanikio.

‎Lakini bado kila siku unaamka bila mpango.

‎Unavua pajama saa nne asubuhi.

‎Unadamkia kucheki status za whatsApp.

‎Halafu mwisho wa siku unaanza kusema: Siku yangu ilikuwa ndefu sana.

‎Bro, HAPANA!

‎Mafanikio hayawezi kumngoja mtu asiye na mpango.

‎Hayawezi kumwangalia mtu anayepoteza siku yake ovyo.

‎Kila siku unachelewa.

‎Kila siku unasema Nitafanya kesho.

‎Kila siku unaweka mipango kichwani bila kuiandika.

‎Na kila jioni unajilaumu kwa sababu siku imepita bila matokeo.

‎Inauma, siyo?

‎Kujua kuwa ungeweza kufanya zaidi… lakini hukufanya.

‎Kujua kuwa ulikuwa na nafasi… lakini uliichezea.

‎Wewe mwenyewe unajua  kuna kitu kinakosekana.

‎Na hicho kitu ni KANUNI YA SIKU YA MAFANIKIO.

‎Siku ya mafanikio haianzi kwa kuamka tu.

‎Inaanza na KANUNI.

‎Mpango.

‎Ratiba.

‎Uamuzi wa kusimama kama mshindi, kila asubuhi.

‎Wengi wanajidanganya:

Wacha tu niende na flow ya siku.

Niache maisha yajiendeshe yenyewe.

‎Hiyo ni NDOTO!

‎Maisha hayaendeshwi kwa flow, bro.

‎Maisha huendeshwa kwa kanuni.

‎KANUNI YA SIKU YA MAFANIKIO ni kama ramani ya kila siku.

‎Unaiandika kabla ya siku haijaanza.

‎Inakuambia:

‎Nani wa kumpigia?

‎Nini cha kufanya saa nne?

‎Ni lipi la kuanza, lipi la kuahirisha?

‎Nini kikikamilika kitakufanya useme: Leo nimefanya kweli!

‎Hii sio ratiba ya kawaida.

‎Ni RAMANI ya mafanikio.

‎Unaiishi. Unaiheshimu. Unaiendea bila kubabaika.

‎Na ikishika… bro, hakuna wa kukuzuia.

‎Kuna time niliamka nikiwa nimechoka kimaisha.

‎Kila kitu kilikuwa kinanichanganya.

‎Mara sipati wateja, mara nashindwa kuandika vizuri, mara stress.

‎Nikagundua tatizo: siku zangu hazikuwa na msimamo.

‎Nilikuwa naamka tu  bila direction.

‎Siku moja nikasema:Leo, natunga kanuni yangu.

‎Nikaandika mambo 3 tu ya muhimu ya kufanya siku hiyo.

‎Nikaanza nayo.

‎Bro, siku ile nilihisi kama nimevaa suti ya Superman.

‎Nilihisi control.

‎Nikapiga simu ya mauzo. Nikaandika content.

‎Nikamaliza kazi kabla ya saa kumi.

‎Na ikaanza kuwa kawaida.

‎Sasa hivi?

‎Kabla siku haijaanza, kanuni iko tayari.

‎Na kila siku huwa na ladha ya ushindi.

‎Ndio maana nakuambia:

‎NDIYO LEO.

‎Anza leo.

‎Tunga kanuni ya siku yako ya mafanikio.

‎Ishi kwa hiyo kanuni kila siku.

‎Na maisha yako yatabadilika kwa kasi ya ajabu.

‎Usisahau:

‎Mafanikio hayaanguki kama mvua.

‎Yanatengenezwa kila siku kwa kanuni, kwa mpango, kwa uthubutu.

‎Na yote yanaanza kwa uamuzi mmoja…
‎NDIYO LEO.

‎Uko tayari?

‎Kama upo tayari, kuipata kanuni yako ya siku ya maneno,

‎Tuma ujumbe NATAKA KANUNI

‎Kwenda 0756694090.

‎Karibu.
‎Imeandikwa Na Mkufunzi Ramadhan.