Tikiti maji  ni tunda ambalo linapatikana kwa wingi sana katika maeneo mbalimbali. Hili ni moja ya tunda ambalo linapatikana kila msimu wa mwaka.

TIKITI

Hata bei ya tikiti maji sio kubwa sana kiasi cha kwamba kila mtu anaweza kupata tunda hili.

Kuna faida nyingi sana za kula tikitimaji. Hapa utazijua faida tano za kiafya.

 

1. Inapunguza magonjwa ya moyo.

Matikiti maji yana kirutubisho ambacho huondoa sumu zinazosababisha magonjwa ya moyo na shinikizo la damu.

2. Ni nzuri kwa mifupa yako.

Kirutubisho hiko kilichopo kwenye matikiti maji kinaweza pia kulinda mifupa na kupunguza magonjwa ya mifupa hasa kwa wazee.

3. Inapunguza mafuta mwilini.

Tafiti zinaonesha kwamba matikiti maji yana virutubisho ambavyo vinazuia mafuta kujikusanya mwilini.

4. Yanaongeza maji mwilini.

Unatakiwa kunywa maji mengi sana kwa siku. Ila ni wachache sana wanaoweza kunywa kiwango kikubwa cha maji. Ukila matikiti maji yanaongeza maji mengi mwilini.

5. Yanaimarisha kinga ya mwili.

Matikiti maji kama yalivyo matunda mengine yana vitamin c kwa wingi ambayo ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha kinga ya mwili.

Hizo ndio baadhi ya faida nyingi za matikiti maji. Ongeza idadi ya vipande unavyokula kila siku ili unufaike zaidi.

TUKO PAMOJA.