Habari za leo rafiki yangu,
Ni matumaini yangu uko vyema na unaendelea kuweka juhudi kubwa ili kuyafanya maisha yako kuwa bora zaidi. Najua unakumbuka ya kwamba mtu pekee wa kuyafanya maisha yako kuwa bora ni wewe mwenyewe, hakuna mwingine anayeliweza hilo. Hili ni jukumu lako ambalo unapaswa kulifanyia kazi kila siku, usilisahau rafiki.

Pia nina imani unajiandaa vyema na semina ya tarehe jumapili hii ya tarehe 30/10/2016 ambapo tutakwenda kujifunza kuhusu kuongeza kipato chako kwa zaidi ya milioni moja.
Kama bado hujalipia tiketi yako ya kushiriki semina hii fanya hivyo leo ili usikose nafasi hii ya kipekee kwako kuweza kupata maarifa na mtazamo sahihi wa kuongeza kipato chako.

Semina itafanyika jumapili hii tarehe 30/10/2016 pale Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza.
Ni kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa 11 jioni.
Gharama ya tiketi ni tsh 35,000/=
Utapata kitabu cha kuandikia, kalamu na chakula cha mchana.
Tutakuwa walimu na wanenaji wanne, ambao nitakuletea sifa zao kesho.

Kulipia tiketi yako tuma tsh 35,000/= kwenye namba 0755 953 887 au 0717 396 253 kisha tuma ujumbe wenye majina yako kamili, namba ya simu na sehemu ulipo.
Fanya hivyo leo hii rafiki yangu, ili usikose nafasi hii ya kipekee kwako kupata maarifa ya kuongeza kipato chako.

Leo nataka kutoa majibu ya maswali ambayo nimekuwa naulizwa na wengi kuhusiana na semina hii ya MILIONI YA ZIADA. Nina imani kupitia maswali haya utapata ufafanuzi wa kutosha popote ambapo hujaelewa.

Swali; vipi kwa sisi ambao tupo mikoani na hatuwezi kuhudhuria, tutapataje mafunzo hayo?

Jibu; kipaumbele cha kwanza kabisa kiwe kuhudhuria semina, kwa sababu kuna nguvu kubwa sana unayoipata kwa kuwa ndani ya ukumbi wa semina kuliko kusoma au kufuatilia mafunzo ukiwa sehemu nyingine. Ndani ya ukumbi wa semina kuna nguvu kubwa ambayo inakuingia na unatoka ukiwa na hatua za kwenda kuchukua, tofauti na unapopata mafunzo kwa njia nyingine, unaweza kuona bado hujawa tayari. Pia unapata nafasi ya kuuliza maswali na kujibiwa moja kwa moja. Bado pia utakutana na watu wapya na hivyo kukuza mtandao wako.
Kama inatokea umebanwa kabisa na hutaweza kuhudhuria moja kwa moja basi utaweza kushiriki semina ambayo tutatoa kwa njia ya mtandao (webinar). Hii ni semina ambayo inaendeshwa moja kwa moja na wewe kufuatilia kwa njia ya mtandao. Utaweza kushiriki semina hii popote ulipo kama ukiwa na mtandao wa intaneti. Kutakuwa na gharama za kushiriki semina hii.

Swali; kwa nini msiandae DVD za semina ili na sisi ambao hatutahudhuria tuweze kupata kile ambacho waliohudhuria wamefanya?

Jibu; kuandaa na kusambaza dvd za masomo haya ni kazi nyingine kubwa ambayo kwa sasa hatutaweza kuifanya. Kazi hii ya kuandaa semina pekee ni kubwa sana, kuandaa na kusambaza dvd itakuwa kubwa zaidi.
Njia bora tuliyoandaa kwa wale watakaokosa ni kushiriki semina hii tutakayoandaa kwa njia ya mtandao.

Swali; je ni kweli nikihudhuria semina hii nitaweza kuongeza kipato changu kwa milioni na zaidi?

Jibu; ndiyo, ukihudhuria semina hii utapata maarifa sahihi  ambayo kama utayafanyia kazi, ninaweza kukudhibitishia kwamba kipato chako kitakua. Tutakwenda kukushirikisha maarifa ya kile ambacho sisi wenyewe tunafanya na mbinu bora zaidi za kuongeza kipato chako kwa kuanzia pale ulipo sasa.

Swali; gharama ni kubwa sana, siwezi kupata punguzo?

Jibu; kwa semina ya siku nzima, zaidi ya masaa nane na unapata chakula pamoja na huduma nyingine, gharama ya tsh 35,000/= siyo gharama kubwa. Ukilinganisha na maarifa utakayopata, naweza kusema huu ni uwekezaji mdogo sana unaofanya, ambao utakuletea marejesho makubwa ukiyafanyia kazi.

Swali; napenda kushiriki semina hii lakini sina fedha ya kulipa ada ya ushiriki.

Jibu; fanya vyovyote uwezavyo (ila usiibe) upate fedha ya kushiriki semina hii. Kwa sababu kama mpaka sasa hujaweza kupata fedha hii ya kushiriki, basi unahitaji sana haya maarifa tunayokwenda kutoa. Kinachokufanya mpaka sasa unakosa fedha ya kuongeza maarifa ya kukuwezesha kuongeza kipato chako, ni kukosa maarifa sahihi na mtazamo sahihi wa kuendesha biashara itakayokuingizia kipato.

Omba, itisha michango na fanya njia nyingine yoyote kupata ada ya kushiriki, fikiria kama umepata dharura ya ugonjwa na lazima upate elfu 35 ungetumia njia gani kupata fedha hiyo? Itumie mbinu hiyo kupata fedha ya kushiriki semina hii.

Nitumie nafasi hii kukukaribisha sana kwenye semina hii kubwa na ya kipekee. Ni semina pekee nitakayotoa mafunzo ya moja kwa moja mwaka huu 2016. Karibu sana tujifunze kwa pamoja.
Pata tiketi yako sasa, tuma fedha tsh 35,000/= kwenye namba 0755 953 887 au 0717 396 253 kisha tuma ujumbe wenye majina yako kamili, namba ya simu na mahali ulipo. Kumbuka zimebaki siku mbili pekee kupata tiketi ya kushiriki semina. Chukua hatua sasa.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,