Habari za leo rafiki yangu?

Karibu tena kwenye kipengele hichi cha makala za ongea na coach ambapo nimekuwa nakuandalia masomo kwa njia ya video. Kupitia masomo haya, nimekuwa nakushirikisha maarifa muhimu sana ya kukuwezesha kupiga hatua kwenye maisha, kuzivuka changamoto na hata kufikia utajiri.

Katika kipindi chetu cha leo tunakwenda kujifunza kuhusu aina kuu mbili za kipato na jinsi ya kuzitumia kufika kwenye utajiri.

Kila mtu huwa anaongelea kuhusu kipato,

Wapo wanaosema kipato hakitoshi, wengine kipato kigumu, wengine wanafikiria kuongeza kipato.

Lakini wote hawa wanazungumzia aina moja pekee ya kipato, ambayo kwa vyovyote vile haiwezi kukufikisha kwenye utajiri na uhuru wa kifedha.

Zipo aina kuu mbili za kipato, aina ya kwanza ni ya kufanya maisha yaende, na aina ya pili ni ya kutengeneza utajiri mkubwa kwenye maisha yako.

Hizi ni aina mbili za kipato ambazo kila mtu ambaye yupo makini na maisha yake anapaswa kuzijua, kuzifanyia kazi na kupata matokeo mazuri.

Kwenye kipindi cha leo nimekushirikisha aina hizi, na kwa mifano kabisa pamoja na namna ya kutumia aina hizo kutengeneza utajiri na uhuru wa kifedha kwenye maisha yako.

Kuzijua aina hizi mbili za kipato na jinsi ya kuzitumia kufikia utajiri, angalia kipindi hichi cha leo.

Unaweza kuangalia kipindi hichi kwa kubonyeza maandishi haya na ukaenda kuangalia. Au kama kifaa chako kinaruhusu, unaweza kuangalia moja kwa moja hapo chini.

Ni imani yangu kwamba utaelewa vizuri aina hizi mbili za kipato na jinsi ya kuzitumia, na kama hutaelewa kwa namna yoyote, niwekee maoni yako chini ya somo hili la leo na nitakupa majibu sahihi.

Jifunze na chukua hatua, kuyaweka yale uliyojifunza kwenye matendo ili maisha yako yaweze kubadilika.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,


Kupata blog yako ya kitaalamu, unayoweza kuitumia kutengeneza kipato, BONYEZA maandishi haya.

Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu

Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.