Habari rafiki?

Karibu kwenye makala yetu ya ONGEA NA COACH ambapo nimekuwa nakushirikisha mambo mbalimbali kuhusu maisha ya mafanikio kwa njia ya video.

Kwenye kipindi chetu cha leo nakwenda kukushirikisha kuhusu kuishinda hofu ya kushindwa.

Ukweli ni kwamba kila mtu anapenda kuwa na maisha bora na yenye mafanikio. Kila mtu anapenda kupiga hatua kwenye maisha yake, anapenda kutoka pale alipo sasa na kupiga hatua zaidi.

Watu wengi hupanga kabisa namna ya kutoka pale walipo sasa, huweka malengo na mipango mikubwa, ambayo ukiisikia, unajua kabisa ya kwamba mtu huyo atakuwa mbali zaidi siku zijazo.

Lakini changamoto kubwa sana inajitokeza pale mtu anapoanza kufanya, pale mtu anapochukua hatua. Hapa ndipo anakutana na vitu vingi vinavyompa kikwazo au sababu ya kwa nini asianze au kuendelea kwa sasa.

Pamoja na sababu nyingi ambazo mtu anaweza kujipa au kukubaliana nao, mzizi mkuu upo sehemu moja; HOFU.

Watu wengi wanashindwa kuanza kutokana na kuwa na hofu. Wengi wanakuwa na hofu kwamba huenda watashindwa, na wakishindwa mambo yatakuwa mabaya zaidi ya yalivyo sasa. Hivyo wanaacha kabisa kuchukua hatua.

Kwenye kipindi cha leo, nimekupa njia tatu muhimu za kuweza kuishinda hofu hii ya kushindwa. Kwa kufanyia kazi njia hizo tatu, kamwe hutoshindwa kuchukua hatua kwenye maisha yako kwa sababu ya hofu. Badala yake hofu itakuwa hamasa kubwa kwako kuchukua hatua.

Angalia kipindi hichi cha leo, ujifunze mambo haya matatu, uanze kuyafanyia kazi na maisha yako yabadilike.

Kuangalia kipindi hichi cha leo, bonyeza maandishi haya. Pia unaweza kuangalia moja kwa moja hapo chini kama kifaa chako kinaruhusu.

Usikubali kabisa hofu ya kushindwa iwe sababu ya wewe kushindwa. Hakuna kushindwa kwenye maisha mpaka pale wewe mwenyewe unapoamua kwamba umeshindwa. Vinginevyo, chukua hatua, jifunze na kuwa bora zaidi.

KWA NINI SIYO TAJIRI

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Makirita Amani,

Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu

Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea www.mtaalamu.net/patablog