#4 TUONGEE PESA; MASHINE YA KUCHAPA FEDHA.
Watu wengi wamekuwa wanahangaika sana kupata njia rahisi ya kutengeneza fedha. Katika harakati hizi wapo ambao wameweza kutengeneza mashine za kutengeneza fedha feki na wengine wamekuwa wanaiba na kutapeli. Njia zote hizo hata kama zitakupa fedha, lakini utatumia sehemu kubwa ya fedha hizo kukimbia au kujificha. Kwa kifupi unaweza kupata fedha, lakini maisha yako hayatakuwa na uhuru wowote.
Ninachotaka kukuambia wewe rafiki yangu ni kwamba unao uwezo wa kutengeneza mashine inayochapa fedha, mashine inayozalisha fedha kadiri utakavyo wewe mwenyewe. Na uzuri wa mashine hiyo ni kwamba ni halali kabisa, na utakuwa huru na fedha utakazozipata kwa sababu huvunji sheria yoyote ile.
Mashine hiyo haihitaji fedha nyingi ili kuitengeneza, ila inahitaji kazi na muda na ukiweza kuitengeneza kwa usahihi, itakuwa inachapa fedha usiku na mchana, ukiwa umelala au umesafiri, mashine inachapa fedha tu.
Je upo tayari kujua mashine hiyo ya kuchapa fedha ambayo unaweza kuwa nayo?
Kama jibu ni ndiyo basi umeshajifunza hapa, kupitia kitabu cha juma hili.
Mashine ya kuchapa fedha ni kuwa na biashara ambayo inaendeshwa kwa mifumo na haitegemei uwepo wako wa moja kwa moja.
Yaani unaanzisha biashara, ambayo umeitengenezea mifumo ya kuendesha biashara hiyo na kuiweka vizuri kwenye biashara hiyo, unapata watu sahihi wa kuendesha mifumo hiyo na mifumo inaleta matokeo mazuri ambayo ni faida.
Mifumo ya biashara ikishakuwa sawa, na ukaweka watu sahihi wa kuendesha mifumo hiyo, hapo unakuwa huru na maisha yako na kazi yako ni kuvuna faida tu. Je hapo siyo sawa na kuwa na mashine ya kuchapa fedha.
Kama una kitu kinachokuingizia fedha ukiwa umelala, umesafiri, unaumwa au unafanya kingine chochote ambacho hakihusiani na kuzalisha fedha, ila fedha zinaingia tu, je hiyo siyo mashine ya kutengeneza fedha?
Na je kwa kupitia haya tuliyojifunza leo, hujaona jinsi ilivyo rahisi kwako kutengeneza mashine hii?
Ninachokuambia ni kimoja rafiki yako, nenda kaweke mifumo kwenye biashara yako, miaka ya mwanzo utahitaji kuweka kazi kubwa, lakini baada ya hapo, utakuwa unavuna tu.
Endelea kusoma makala ya TANO ZA JUMA kujifunza njia bora za kuendesha biashara inayokupa uhuru na mafanikio makubwa. Soma zaidi hapa; Tano Za Juma Kutoka Kitabu; THE E-MYTH REVISITED, (Kwa Nini Biashara Nyingi Zinashindwa Na Hatua Za Kuchukua Ili Biashara Yako Isishindwe).
FURSA YA KUTENGENEZA BIASHARA YAKO KWA MFUMO.
Rafiki, kama umejifunza hapa kuhusu faida na jinsi ya kuendesha biashara yako kwa mfumo, na umeona ni kitu ambacho unahitaji ili kufanikiwa, basi nakukaribisha tufanye kazi pamoja ya kukuwezesha kutengeneza biashara yako kwa mfumo.
Ninayo programu ambayo nafanya kazi na wafanyabiashara ambao wanaendesha biashara zao kwa mfumo rahisi kwao kuzifuatilia na kupata watu sahihi pamoja na kupanga na kupima ukuaji wa biashara hiyo.
Kama unataka kuwa mmoja wa wafanyabiashara waliopo kwenye programu hii, basi nitumie ujumbe kwa njia ya wasap namba 0717396253 kwenye ujumbe andika PROGRAMU YA KUENDESHA BIASHARA KWA MFUMO, na nitakutumia maelekezo ya programu hiyo.
Karibu sana.