“The difference between real material poison and intellectual poison is that most material poison is disgusting to the taste, but intellectual poison, which takes the form of cheap newspapers or bad books, can unfortunately sometimes be attractive.” – Leo Tolstoy

Kuna aina mbili za sumu kwenye maisha,
Kuna sumu ya mwili, hii ni ile ambayo ukiitumia inaleta madhara ya haraka.
Sumu hii ni chungu mdomoni na haivutii, hivyo wengi huikwepa.
Halafu kuna sumu ya akili, hii hi ile ambayo inajipenyeza kwenye fikra za mtu, kuharibu mtazamo wake na mwisho maisha yake.
Sumu hii huwa ni tamu na ya kuvutia kwenye akili, ni habari za udaku, habari mpasuko, mambo ya wengine na habari nyingine za aina hiyo.
Sumu hii imekuwa na madhara kwa wengi, lakini wao wenyewe wamekuwa hawajui.

Mwaka 2020 ni mwaka muhimu kwetu kuepuka sumu hii tamu na ambayo imekuwa na madhara kwetu kwa miaka mingi.
Huu ni mwaka wa kuondokana na taarifa na maarifa yasiyo na maana.
Chujio letu la taarifa au maarifa ni mwongozo wetu wa AFYA, UTAJIRI NA HEKIMA, kama taarifa au maarifa hayana mchango kwenye vitu hivyo vitatu, achana nayo, ni sumu kwako.

#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma

Tuwe na usiku mwema, wa kuitafakari siku tuliyoimaliza na kupangilia siku inayofuata.
Kocha Dr Makirita Amani.