#SheriaYaLeo (349/366); Ondoka kwenye mazoea na kuiga.

Huwa tunaiangalia dunia kwa kutumia mazoea na kuiga wengine.
Tunafanya yale tuliyozoea kufanya au tunayowaona wengine wakifanya.

Kuna mengi ambayo tunashindwa kuyang’amua kutokana na mazoea tunayokuwa nayo.
Hayo yanatutaka kwenda zaidi ya mazoea na kuiga.
Yanatutaka tutumie uwezo mkubwa ulio ndani yetu kuweza kutang’amua.

Ili kuweza kuielewa dunia na kung’amua mengi yanayotuzunguka, tunapaswa kuachana na mazoea na kuiga, badala yake tunapaswa kuzama kwenye jambo linalokuwa mbele yetu na kutumia uwezo mkubwa ulio ndani yetu kuweza kulielewa.

Tunapaswa pia kufanya mambo ambayo hatujawahi kufanya au kwenda maeneo ambayo hatujawahi kwenda ili kuvunja mazoea ambayo tulishajijengea.

Tumia kila fursa ili kuweza kuondokana na mazoea na kuikabili dunia jinsi ilivyo badala ya kuikabili kama ulivyo wewe.

Sheria ya leo; Huwa tunahofia kuikabili dunia kama ilivyo kwa sababu ya ukubwa wake. Hivyo tunakaa kwenye mazoea na kuiga wengine. Hayo yanatupa ukomo ambao unatuzuia kufanya makubwa. Tunapaswa kuondoka kwenye hayo mazoea na kuiga ili kuweza kutumia uwezo wetu mkubwa kuielewa na kuitumia dunia.

#NidhamuUandilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji