2958; Abiria ambao hawaendi Arusha washuke.
Rafiki yangu mpendwa,
Pata picha wewe ni dereva wa basi ambalo linafanya safari zake kutoka Dar kwenda Arusha.
Basi imepaki kwenye stendi kuu ya mabasi ya Dar na kupakia abiria.
Basi inajaa kisha unaanza safari.
Ile unatoka tu kwenye stendi na kuelekea kibaha, kundi la abiria wanaanza kupiga kelele basi linaenda wapi.
Wanaeleza kwamba wao wanaenda Mtwara, kwa huo uelekeo wako siyo sahihi.
Unashangazwa ni kwa namna gani abiria hao wa Mtwara wamekuwa ndani ya basi la Arusha.
Kunakuwa na mvutano, hawataki kushuka kwa sababu hawataki kusumbuka tena kupata basi nyingine.
Wanachotaka ni basi igeuke na kuelekea upande wa Mtwara.
Unafanya kila namna kuwashawishi washuke, unawapa mpaka fidia. Baada ya mzozano mrefu, wanakubali kuchukua fidia na kushuka.
Unaona ahueni na safari inaendelea, japo sasa kwa kuchelewa.
Unaendesha mpaka Chalinze.
Ile unakatisha kona kwenda uelekeo wa Tanga, kundi jingine la abiria wanaanza kupiga kelele gari inaelekea wapi?
Abiria hao wanasema wanaelekea Mbeya hivyo basi inapaswa kuwa na uelekeo wa Morogoro.
Mnaanza upya majadiliano na abiria hao, ambao hawataki kusikia habari nyingine zaidi ya basi kwenda uelekeo sahihi.
Unawashawishi washuke, kitu ambacho hawapo tayari maana wanasema itawawia vigumu kupata basi.
Inakubidi uingie wajibu wa kuwatafutia basi ndiyo wakakubali kushuka.
Mpaka hatua hiyo, kama ni dereva makini itakubidi utoe tangazo kwa abiria wote.
Kwamba kama kuna abiria ambao hawaendi Arusha wanapaswa kushuka kwenye basi hilo.
Abiria hao wameingiaje kwenye basi hilo siyo kitu cha kusumbuka nacho sana katika hatua hiyo.
Maumivu makubwa ni safari inachelewa kutokana na kuwa na abiria wasio sahihi ndani ya basi.
Japokuwa wewe siyo dereva wa basi, ni dereva wa maisha yako, kazi na hata biashara yako.
Una abiria wengi kwenye kila basi lako na wengi ambao hawaendi unakoenda.
Tukiangalia basi la biashara yako ambalo wewe ndiye dereva, kuna abiria wa aina mbalimbali.
Kuna abiria ambao ni wafanyakazi, wengine wateja, wapo wasambazaji na washirika mbalimbali.
Katika watu hao, kuna ambao wana maono kama uliyonayo na mna uelekeo unaofanana. Hawa mnaendana vizuri.
Lakini kuna ambao mnatofautiana maono na hata mwelekeo.
Hawa mnakuwa na misuguano mingi inayochelewesha safari.
Unapaswa kufanya maamuzi sahihi kwa kuwaondoa abiria wote wasio sahihi kwenye basi lako.
Kwa wateja ni kuachana na wateja wote wasio sahihi kwa biashara yako.
Kwa wafanyakazi ni wale ambao hawakidhi vigezo vilivyopo.
Kadhalika kwenye maeneo mengine, wale ambao uelekeo wao ni tofauti na wa biashara, wanapaswa kuondolewa.
Ni zoezi gumu kufanya na wakati mwingine linapunguza kipato chako.
Lakini kwa muda na nguvu unazopoteza kuhangaika na abiria hao wasio sahihi, maamuzi ya kuwashusha yanakuwa bora zaidi.
Anza kwa kuwashusha abiria wasio sahihi, ambao uelekeo wao ni tofauti na wako.
Halafu kazana kupakia abiria walio sahihi, kwa kueleza wazi basi yako inaelekea wapi na watu wa aina gani unahitaji.
Bila ya kuwa na msimamo huu, hakuna hatua kubwa utakayoweza kupiga.
Uelekeo wa safari mmoja, abiria unaohitaji ni wale wenye uelekeo huo.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Nitashusha kila abiria asiekwenda niendako
Asante sana kocha
LikeLike
Nitashusha abiria wote wasio sahihi ni zoezi endelevu
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Asante sana Kocha, uelekeo sahihi wa biashara yangu Ni kitu muhimu Sana, tofauti na hapo nitayumbishwa Sana.
LikeLike
Asante Sana. Abiria ambao hawawezi KWENDA kwenye Basi langu washukr
LikeLike
Asante sana ni sahihi sana hilo ni muhimu sana kwasababu ni dhahili ni muhimu kufanya maamuzi ya muhimu.
LikeLike
Asante kocha,ninapaswa kuwa na watu sahihi kwenye biashara yangu,sio kukaa na watu ambao hawajui tunataka nini na nini kusudi letu kwenye biashara.
LikeLike
Kwa wale watu wasio na muelekeo mmoja nmi ambao ni kuelekea kwenye ubulionea na muhimu zaidi kuwaacha.
LikeLike
Abiria ambao HAWAENDI NA LUPYANA BUSINESX washuke
Kweli kabisa kocha biashara zetu zona abiria ambao wanatuchelewesha maana HAWAENDI njia Moja na sisi. Wakati mwingine mwanzoni tunawaona ni wenzetu , lakini kumbe walifika Chalinze watatKa kuelekea Morogoro. Bora kujua tangu mwanzo kwamba Hawa ni WA Mtwara. Kuliko ukaenda nao muda mrefu na kuwazoea kumbe wao wanaenda Mbeya na sio Arusha.
Asante kocha.
LikeLike
Kabisa, ijulikane mapema kabisa.
LikeLike
Tuajiri watu wenye kuyajua na kuyaishi maono ya biashara zetu ndiyo zitakua na kudumu.
LikeLike
Hakikia nitahakikisha nawaondoa abiria wote ambao wanaenda tofauti na maono ya biashara yangu, maisha yangu na kwenye malengo yangu kiujumla.
Ahsante sana kocha kwa funzo hili la leo
LikeLike
kuwashusha abiria wasio sahihi kwenye kila nyanja ninayojihusisha nayo ni maamuzi magumu yanaumiza lakini ndiyo sahihi kufanya kuokoa uelekeo nisipotee.
Muhimu zaidi nikuwashusha hamna namna.
LikeLike
Asante Sana kocha,kuna umuhimu wa kuwatangazia abilia wote washuke yaani kama wafanyakazi hawapo tayari kufundishika wanatakiwa kutafuta basi jingine,wanatakiwa kutafuta kazi nyingine ya kufanya au sehemu nyingine ya kufanyia kazi.
LikeLike
Hakuna namna lazima niwashushe tu, nafikiri Hawa siyo abiria Maana hata tiketi ya kule wanakoelekea hawana. Lift waliyopata inawatosha Hadi sasa. Abiria Halisi nitakayemjali ni yule mwenye tiketi ya mwisho wa safari anayoelekea.
LikeLike
Unapaswa kufanya maamuzi sahihi kwa kuwaondoa abiria wote wasio sahihi kwenye basi lako.
LikeLike
Abiria wasiokwenda Arusha washuke.
LikeLike
Ni kazi kubwa luwashusha abiria wasio na uelekeo wa gari. Japo Kuna woga na hasara ya fidia inayoweza kutumika lkn AMBAO HAWAENDI ARUSHA WOTE NAPIGA CHINI maramoja.
LikeLike
Mimi ni dereva wa maisha, kazi na biashara yangu ABIRIA WOTE WASIOKWENDA SAWA SAWA NA MAONO YANGU NAWAPIGA CHINI MMOJA BAADA YA MWINGINE.
LikeLike
Nitakaa kwenye basi sahihi na kuepuka kumsumbua dereva, nitapakia abiria Sahihi na watakaopakia kimakosa nitawashusha haraka kuokoa muda.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Dawa ni moja, kuwashusha abiria wasio sahihi, ambao uelekeo wao ni tofauti na wangu.
Halafu kuanza kupakia abiria walio sahihi.
Ahsante sana Kocha.
LikeLike
Asante sana Kocha, abiria ambao wamepotea basi lakupanda lazima washushwe. Nimeshaanza kufanya utekelezaji. 🙏🏽
LikeLike
Kubwa kama dereva kwenye maisha yangu na biashara yangu napaswa kujua kule ninakoelekea na kuangalia je wale ninaojihusisha nao wanaelekea huko huko ninapokwenda.Kama sio ni bora kuachana nao mapema.
LikeLike
Ni kuwa na sifa za watu unaosafiri pamoja la sivyo watakushusha njiani, maana hamuendi uelekeo mmoja.Asante Sana kocha.
LikeLike
Ni muhimu kujua na sifa za watu unaosafiri pamoja ili kuendana nao, la sivyo watakushusha njiani, maana hamuendi uelekeo mmoja.Asante Sana kocha.
LikeLike
Asante Kocha napaswa kuwa na uelekeo sahihi kabla ya safari.
LikeLike
Washuke
LikeLike
Asante sana kocha kwa somo hili.
LikeLike