Rafiki yangu na msomaji mzuri wa AMKA MTANZANIA bwana Jiduma Luhende kitambo kidogo alinitumia kitabu hiki kinachoitwa Why You’re Dumb, Sick And Broke kilichoandikwa na Randy Gage.

Baada ya kukisoma kitabu hiki nimejifunza mambo mengi sana kwa nini ujinga, maradhi na umasikini tunavikaribisha sisi wenyewe. Ujinga, umasikini na hata maradhi yanayokusumbua wewe umeyakaribisha wewe mwenyewe kwa mawazo uliyoweka au uliyowekewa kwenye kichwa chako.

Kitabu hiki kinaelezea ni jinsi gani jamii imejenga picha hasi kuhusu utajiri, vyombo vya habari na hata tamthilia mbalimbali zinaonesha utajiri kama kitu kibaya sana na matajiri kama watu ambao maisha yao hayana furaha na wabinafsi wenye roho mbaya. Picha hii tunayoingiziwa kila siku inatufanya tuone umasikini ndio wenye furaha na roho nzuri.

dumb

Kitabu hiki pia kimeeleza ni jinsi gani dini mbalimbali tunazoamini zinatutengeneza kuwa masikini. Ameeleza kwa mifano mizuri sana mambo yanayofanyika kwenye dini kwa kujua au kutojua lakini yanakufanya wewe uone ni vizuri kuwa masikini kuliko kuwa tajiri.

Kitabu hiki hakikuacha nyuma mchango wa serikali kwenye kukufanya wewe uwe mjinga na masikini. Serikali ina mpango mzuri sana wa kuhakikisha wewe unaendelea kuwa mjinga na masikini ili uendelee kuitegemea kwa kila kitu na usiwe na nguvu ya kuihoji. Kwa njia hii serikali nyingi duniani zinaadhibu wenye fedha nyingi na utajiri na kubembeleza wale ambao ni masikini.

Kuna mambo mengi sana kwenye kitabu hiki ambayo ukiyasoma utabadili kabisa mtazamo wako juu ya maisha yako kuhusu utajiri na umasikini.

Katika kitabu hiki mwandishi ameshauri biashara tatu ambazo mtu anaweza kuzifanya na akawa na uhuru wa kifedha. Tatizo kubwa la biashara nyingi ambazo watu wanafanya ni kwamba inakuwa vigumu sana biashara kujiendesha zenyewe bila ya uwepo wa mmiliki kwa asilimia kubwa. Hii inakufanya wewe mmiliki wa biashara kupoteza umiliki wako, badala ya wewe kumiliki biashara, biashara inakumiliki wewe.

Mwandishi ameshauri biashara tatu ambazo kati ya hizo mbili unaweza kuzianza ukiwa na mtaji kidogo ila baadae ukajenga biashara kubwa sana ambayo haitakumiliki. Sitakuambia biashara hizi hapa, soma kitabu hiki halafu ukishafikia ambapo mwandishi ameshauri kuhusu biashara hizi niandikie email kwenye amakirita@gmail.com kuniambia ulivyozielewa biashara hizo kisha nitakushauri na kukupa mwanga zaidi kuhusu biashara moja au mbili kati ya hizo ambayo ndio nafanya kila siku na inaonesha mafanikio makubwa. Kwa kusoma kitabu hiki na kupata ushauri huo juu ya biashara unaweza kupata fursa kubwa sana kwenye maisha yako ambayo itayabadili kabisa maisha yako.

kitabu kava tangazo

Nakusihi sana usome kitabu hiki, ni kitabu kifupi ambacho kinaeleweka haraka sana. Kitabu hiki kina kurasa zisizozidi 190 zenye maandishi, kama ukiamua kukisoma kwa nusu saa kila siku, baada ya wiki moja utakuwa umekimaliza na umejifunza mengi sana.

Kama utakisoma kitabu hiki mpaka mwisho utajua kwa nini wewe ni MJINGA, MASIKINI NA MGONJWA na utajua ni jinsi gani ya kuwa MJANJA, TAJIRI na AFYA NJEMA.

Angalizo, wakati unasoma kitabu hiki inabidi uwe na uwezo wa kuhoji kila unachokisoma, ndivyo mwandishi alivyokiweka kitabu hiki. Kinakuchochea uwe na uwezo wa kuhoji kila kitu kwenye maisha yako, kuanzia kazi unayofanya, wanaokuzunguka, dini yako, habari unazopata na hata serikali yako. Hivyo kama wewe ni mvivu wa kuhoji unaweza kuona kitabu hiki kinakufundisha uasi hasa linapokuja swala la dini au watu wanaokuzunguka.

Kitabu hiki kimetumwa kwa wanachama wa mtandao huu. Kama bado hujawa mwanachama na ungependa kupata kitabu hiki bonyeza maandishi haya na uweke email yako na uweke email yako kisha ujiunge na utatumiwa email yenye link ya kitabu hiki pamoja na vitabu vingine viwili.

Nakusihi tena soma kitabu hiki, hakuna utakachopoteza ila utakuwa na kila kitu cha kujifunza.

Nakutakia kila la kheri kwenye safari yako ya kuboresha maisha yako.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali endelea kuwaalika marafiki zako kulike page yetu ya facebook. Bonyeza maandishi haya na kisha like halafu nenda sehemu ya invite friends kisha waalike nao walike ukurasa huu ili tuweze kuwafikia wengi zaidi. Asanye sana kwa ushirikiano wako.