Kwa wale ambao ni wazazi bila shaka wanajua malezi bora ni kitu cha msingi sana katika makuzi ya mtoto. Na malezi haya bora huwa hayaji tu kwa bahati mbaya, bali hujengwa hatua kwa hatua kwa kadri jinsi mtoto anavyokua.
Kwa kujua umuhimu wa hilo, hebu leo kupitia makala haya tuangalie hatua nyingine muhimu ya malezi kwa kujifunza njia nyingine za kumfanya mtoto wako ajione ni wa pekee. Je, njia hizi ni zipi? Fuatana nami kujifunza kupitia makala haya.
1. Tenga muda wa kua nae pamoja.
Unaweza ukamfanya mtoto wako akajiona wa pekee kwa kutenga muda wa kuwa nae. Muda huu unaweza kuutenga kwa kuwa na mtoto wako jioni unapokuwa  nyumbani au wakati mwingine kutembelea maeneo kama ‘beach’, mbuga za wanyama au makumbuso.

Kwa hiki kipindi kinakuwa ni muhimu sana kwako na mtoto wako kwa sababu, hapa mtoto anakuwa anajifunza mambo mhumu kutoka kwako. Kwa kifupi, hiki ni kipindi muhimu kwa mtoto kwa sababu anakuwa anajihisi ni wa pekee sana kwa kuona anajaliwa zaidi na wazazi, hasa kwa kuwa karibu nao.
2. Msikilize kile anachokisema.
Kuna wakati watoto wetu huwa wanapenda sana kutoa maoni yao. Inapotokea mtoto wako anakupa maoni ya kitu fulani, msikilize kile anachokisema, kisha msifie hata kama hayupo sahihi, lakini baada ya hapo kama ni kweli hayupo sahihi, chukua jukumu la kumrekebisha.
Kwa kufanya hivi kutamfanya mtoto wako atakuwa anakushirikisha mambo mengine mengi na kujiona wa pekee. Hiyo itamuongezra nguvu kubwa ya kujiamini kadri siku zinavokwenda. Na kwa mwendo huo unakuwa umemtengenezea ujasiri mkubwa utakao dumu kwa baadae.
3. Jali kile anachokijali mtoto wako.
Ikiwa moto wako anaonyesha anajali mchezo wa aina fulani, muunge mkono kama mchezo huo ni wa maana. Haimaanisha kujali huku, ujali kila kitu hapana. Kama pengine mchezo huo hauna maana mweleze na umtafutie kitu kingine.
Ili kuonyesha unajali zaidi, endelea kumdadisi ni kitu gani kingine anapenda au ni mchezo gani mwingine anaoupenda. Hapa utakuwa unamfanya mtoto wako azidi kujiona ni wa pekee kwako mzazi kwa kuwa unajali hisia zake na unazielewa.
 4. Mtengenezee utamaduni bora.
Pia njia nyingine ya kumfanya mtoto wako ajione wa pekee ni kule kumjengea utamaduni wako unaoupenda. Pengine unajiuliza ni utamamduni wa naman gani sikiliza, unaweza kujengea utamaduni wa kujiamini na kufikiri chanya.
Utafanikisha hili ikiwa utakuwa una mpa moyo na nguvu kwa yale anayoyafanya. Hiyo haitoshi kama anauwezo wa kusoma vizuri, unaweza ukampa vitabu vizuri vya kusoma vinavyozungumzia mambo chanya.
5. Muulize mambo muhimu.
Pia mjengee mtoto wako utaratibu wa kumuuliza mambo muhimu. Kwa mfano, ‘unapenda nini mwanangu, ukiwa mkubwa unataka kufanya nini,’ na mengineyo mengi maswali ya kidadisi. Hii itakuwa ni njia nzuri pia ya kumfanya toto wako afikiri vizuri na upya.
Kwa kuhitimisha, hizo ni baadhi ya njia ambazo unaweza ukazitumia na kumfanya mtoto wako ajione wa pekee na kufurahia maisha kwa ujumla.
Endelea kutembelea http://www.amkamtanzania.com kujifunza kila siku.

Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,