Binadamu huwa tuna tabia ya kujitengenezea utumwa wetu wenyewe.
Tunaanza kufanya vitu kwa sababu ambazo hatuzijui, na baadaye tunajikuta tunaendelea kufanya vitu hivyo maisha yetu yote.
Hivyo mtu unakuwa umetingwa kweli na vitu unavyofanya, lakini hata siku moja hujawahi kukaa chini na kujiuliza kwa nini unafanya.
Hivyo unajikuta unafanya kwa mazoea, kwa sababu ndiyo kitu ambacho umekuwa unafanya mara zote.
Au unajikuta unafanya kwa sababu kila mtu anafanya au kila mtu anakutegemea ufanye.
Au unafanya kwa sababu ya uvivu wako.
Inawezekana pia unafanya kwa sababu ya majuto uliyonayo.
Na kwa wengi, unajikuta unafanya kwa sababu ya tamaa zako.
Misukumo yote hii ya kufanya siyo sahihi na ndiyo maana watu wanafanya mambo mengi, wanachoka kweli lakini hakuna hatua wanazopiga kwenye maisha yao.
Unahitaji kuwa na sababu kubwa ya chochote kile unachofanya, sababu iliyo nje yako kabisa, sababu ambayo ina manufaa makubwa kwako na kwa wengine pia.
Hivyo kwa kila unachofanya, anza kwanza kujiuliza kwa nini unakifanya na usiendelee kufanya mpaka pale unapokuwa umepata sababu sahihi ya kufanya, sababu kubwa zaidi yako.
Fanya kitu kwa sababu ndiyo kitu sahihi kufanya na kina manufaa makubwa kwako na kwa wengine pia. Nje ya hapo, utakuwa unafanya kitu kwa sababu binafsi ambazo ni vigumu sana kukufikisha kwenye mafanikio makubwa.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Dr. Makirita Amani,
Asante sana kocha
Kila jambo ninalofanya nitafanya kwa manufaa yangu na wengi8pia
LikeLike
Vizuri Mary,
Kila la kheri.
LikeLike