Habari za leo rafiki yangu?
Karibu kwenye makala yetu ya leo katika mtandao wako wa mafunzo na hamasa AMKA MTANZANIA. Kama ambavyo umekuwa unategemea, kupitia mtandao huu unapata maarifa yanayokuwezesha wewe kufanya maamuzi sahihi ya maisha yako. Ninaweza kukuahidi ya kwamba utaendelea kupata maarifa haya kila siku.

Leo nataka tujadili na kugusia kidogo jinsi unavyoweza kuanzisha biashara, kutoka sifuri mpaka faida ya mamilioni.
Najua swali la kwanza utakalojiuliza, hasa kama bado hujaingia kwenye biashara ni je inawezekana? Na mimi nitakujibu, ndiyo inawezekana, tena sana.

Swali la msingi unalohitaji kuuliza ni je nawezaje kuanza biashara kutoka chini mpaka kufika faida ya mamilioni? Na hapo ndipo tunaweza kujadili kwa kina, na kukuonesha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kufanya hivyo.
Kuna maswali ambayo inabidi uache kujiuliza, kwa sababu yanakupoteza kwenye safari yako ya kuanzisha na kukuza biashara yako. Baadhi ya maswali hayo ni kama;

Ninahitaji kwenda wapi ili niweze kuanzisha biashara hiyo itakayokuwa kubwa? Swali kama hili linakupoteza kwa sababu huhitaji kwenda sehemu fulani ya tofauti ndiyo uweze kuanzisha biashara yako, badala yake unaweza kuanzisha biashara hapo hapo ulipo sasa na kuweza kuikuza zaidi. Kujiuliza unapaswa kwenda wapi ni kupoteza muda wako, kwa sababu muhimu siyo pale ulipo, bali muhimu ni kile kilichopo ndani yako.

Kipi kilicho ndani yako ambacho ni muhimu katika kuanzisha na kukuza biashara yako?

Hapa ndipo muhimu, hapa ndipo unapata majibu ya maswali na changamoto zako. Kinachopaswa kuwa ndani yako, ambacho kitakuwezesha kuanzisha na kukuza biashara yako ni maarifa sahihi na mtazamo sahihi.

Ndiyo, vitu viwili muhimu sana, maarifa sahihi na mtazamo sahihi juu yako binafsi, biashara unayofanya na biashara kwa ujumla.
Kwa kifupi ni kwamba, ili uweze kubadili maisha yako, ili uweze kuanzisha na kukuza biashara yako, huhitaji kwenda sehemu ya tofauti, bali unahitaji kupata maarifa na mtazamo tofauti.

Na hapa ndipo nakupa fursa nzuri sana na ya kipee kwako kupata maarifa sahihi na mtazamo sahihi wa kuanzisha biashara na kuikuza. Hapa ndipo nakukaribisha kwenye mafunzo ya kipekee sana, ambayo yatakutoa hapo ulipo kimaarifa na kifikra, na kukupeleka hatua nyingine, ambayo itakuwa bora sana kwako.
Karibu kwenye semina ya MILIONI YA ZIADA, kwenye semina hii nitakufundisha hatua kwa hatua na kwa mifano, jinsi unavyoweza kuanzia biashara chini kabisa, yaani sifuri na kuikuza mpaka kufikia faida ya mamilioni.

Mwalimu na rafiki yetu Felix Maganjila, atafundisha jinsi ya kuikuza biashara ambayo kwa sasa imedumaa au haipigi tena hatua. Hapa utapata maarifa na mtazamo sahihi wa kuirudisha biashara yako kwenye uelekeo sahihi.
Watakuwepo walimu wengine pia, watakaokupa maarifa sahihi ya kuanzisha na kukuza biashara zao.

Karibu sana kwenye semina hii, naweza kukuhakikishia kitu kimoja, hutatoka kama ulivyoingia, bali utatoka ukiwa mtu wa tofauti, ambaye ataweza kuyatumia mazingira yake kufanya makubwa.

Semina hii itafanyika jumapili ya wiki hii, tarehe 30/10/2016 pale Blue Pearl, ubungo plaza. Ni semina ya siku nzima ambapo utapata mafunzo yote muhimu, ukitoka unakuwa wa tofauti kabisa.
Kiingilio kwenye semina hii ni tsh 35,000/= kwa tiketi moja. Utapata kalamu na kitabu cha kujiandikia, chakula cha mchana na vitu vingine.

 Ili kuweza kuweka mipango vizuri, na kuhakikisha semina hii inakupa thamani unayotegemea kupata, mwisho wa kulipia na kupata tiketi za semina hii itakuwa siku ya ijumaa tarehe 28/10/2016. Hivyo zimebaki siku 4 pekee za kupata fursa hii ya kipekee ya kuanzisha na kukuza biashara yako.

Kama hupendi kukosa fursa hii, nakushauri sana ulipie tiketi yako mapema. Kupata tiketi tuma ada hiyo ya kushiriki kwenye namba 0717 396 253 au 0755 953 887 kisha tuma ujumbe wenye majina yako kamili pamoja na mawasiliano yako. Chukua hatua leo rafiki, hustahili kukosa maarifa haya ya kipekee sana kwako.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kwa ushauri na Coaching bonyeza maandishi haya kupata utaratibu.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea MTAALAMU NETWORK