Wengi tunajua michezo ya bahati nasibu na wengi wetu tumewahi kucheza michezo hiyo. Kwa hapa tanzania iikuwepo michezo mikubwa ya bahati nasibu kama jackpot bingo, lotto kitita na mingineyo. Kwa sasa michezo hii inachezeshwa sana na makampuni mbalimbali kuongeza mauzo ya bidhaa zao. Makampuni ya simu na vileo ndio kwa sasa yanaendesha michezo mingi ya aina hii.

bahati

  Kwenye bahati nasibu yoyote huwa wanashiriki watu wengi sana. Ila mshindi huishia kuwa mmoja ama watatu waliobahatika. Wengine hakuna atakaefahamu kama hata walishiriki bahati nasibu hiyo. Kuna uwezekano umeshiriki bahati nasibu nyingi sana, ila kama hujawahi kuwa kati ya wachache waliobahatika kushinda basi hakuna anaejua kama hata ulishiriki.

bahati2

  Jamii inayotuzunguka haina tofauti na mfumo wa bahati nasibu. Unaweza kuwa unafanya jambo zuri ila kama halionekani ama halijaigusa jamii basi hakuna atakaejua kama unafanya jambo lolote.

  Usikate tamaa kama hakuna anaekuona sasa hivi, endelea na mipango yako na mwisho wa siku itadhihirika kwa kila mtu.

  Hakuna mtu aliefanya mabadiliko na yakaanza kunekana mara moja, mabadiliko mengi huchukua muda kueleweka hivyo usikate tamaa.

  Hakikisha unaleta mabadiliko kwenye kile unachofanya iwe biashara ama ajira. Yafanye maisha ya binadamu yawe rahisi na yakufurahia. Usikate tamaa kama hakuna anaekuelewa kwa sasa, ndivyo jamii ilivyo.